Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Thursday 6 September 2012

Nape awashukia CHADEMA


NA PETER KATULANDA, MWANZA
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimewataka viongozi wa CHADEMA kuheshimu vyombo vya sheria na kuwajibika kisiasa, hasa kutokana na mfululizo wa matukio ya mauaji na kujeruhi watu katika mikutano ya operesheni za chama hicho.
Pia, imevitaka vyama vya siasa na wanasiasa, kujenga utamaduni wa kuheshimu utawala wa sheria, kulinda amani na utulivu uliopo nchini ili tamaa na uchu wa madaraka usiendelee kupoteza maisha ya wananchi.
Wito huo ulitolewa jana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM Taifa, Nape Nnauye, alipozungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali jijini hapa.
Nape alisema katika operesheni za chama hicho Septemba 2, mwaka huu, mkoani Iringa, zilijitokeza vurugu zilizosababisha kuuawa kwa mwanahabari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi na kujeruhiwa vibaya kwa askari watatu wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU).
Alisema Chama kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo hicho cha mwandishi huyo wa habari na kujeruhiwa kwa askari hao.
Nape alisema CCM inachukua nafasi hiyo kutoa pole kwa wafiwa, wanahabari nchini na wote walioguswa na msiba huo na kutoa wito kwa tume zilizoundwa kuchunguza suala hilo, akitaka zichunguze tukio hilo kwa umakini na weledi ili kubaini chanzo cha vurugu hizo na mazingira ya kifo cha Mwangosi.
Hata hivyo, aliomba uchunguzi huo ufanyike kwa muda mfupi ili ukweli uweze kubainika mapema na hatua zinazostahili zichukuliwe bila upendeleo kwa wahusika.

“Unaponyooshea wenzako kidole wawajibike, anza na wewe, matukio haya si mazuri kutokea mara kwa mara kwenye shughuli za chama cha siasa, ni aibu inayohitaji uwajibikaji hata kama ni ya kisiasa,” alisema Nape na kuongeza viongozi wa CHADEMA wana roho ngumu na ujasiri usio wa uwajibikaji.
“Hatutetei upande wowote, tunataka tamaa ya madaraka isipoteze maisha ya watu... CCM imesikitishwa mno na mfululizo wa watu kupoteza maisha au kujeruhiwa katika mikutano na operesheni mbalimbali zinazoendeshwa na CHADEMA nchini, hasa zilizofanyika kwa kukaidi amri halali ya vyombo vya ulinzi na usalama,” alisema.
Katibu huyo aliyataja matukio mengine ambayo CHADEMA imesababisha vurugu na mauaji kuwa pamoja na lile la kuuawa kwa kada wa CCM mkoani Singida na hivi karibuni mkoani Morogoro, ambapo Ally Hassan aliuawa.
“Matukio haya sio mazuri kwa chama cha siasa, kwa nini wanaopoteza maisha ni wengine na siyo wale wanaozianzisha?” alihoji Nape na kuongeza mstaarabu wa siasa angeachana na siasa za kupoteza maisha ya watu, kwani watu hao hawarudi.
Akifafanua, alisema vifo hivyo vimekuwa vikisababishwa na chama hicho kutotii amri halali zilizotolewa kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi ambayo ni ile ile iliyovipa uhalali vyama vya siasa kuwepo na kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa Katiba na si uroho na matakwa ya wanasiasa wake.
Alisema CHADEMA ingesubiri siku chache zilizobaki kabla ya mchakato wa sensa kumalizika ndipo kiendelee na mikutano yake, hivyo mauaji hayo yasingetokea, lakini kimekuwa kikikebehi na kukaidi amri za polisi kwa kauli za ‘tupo tayari kwa lolote’, jambo ambalo ni ishara ya kujiandaa kwa fujo hizo.
Katibu huyo alisema kwamba kwa kuwa CCM inatii amri halali za vyombo vya serikali, ndiyo maana iliahirisha mikutano yake ya hadhara iliyokuwa ifanyike katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo mkoani Kigoma.

Friday 23 March 2012

rais kikwete afunga maonesho ya maadhimisho ya wiki ya maji kitaifa mkoani iringa leo

 Mto Ruaha ukionekana kutoka juu ukitiririsha maji ambao Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuchukua hatua madhubuti za kuunusuru mto huo dhidi ya uharibifu ili kuleta tija zaidi katika kilimo cha umwagiliaji na uzalishaji umeme.Rais Kikwete ametoa ahadi hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji iliyofanyika kitaifa Mkoani Iringa .
Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji kilichofanyika kitaifa katika uwanja wa Michezo wa Samora mkoani Iringa

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia bustani ya mfano inayotumia utaalamu wa kumwagilia kwa matone(drip Iririgation) wakati wa maonyesho yaliyofanyika katika Uwanja wa michezoi wa Samora mkoani Iringa
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya jinsi ya kutibu maji kutoka kwa mtaalamu wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho katika uwanja wa michezo wa Samora mjini Iringa. Picha na Freddy Maro 
Rais Jakaya Kikwete akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa Maji Vijijini Wizara ya Maji na Umwagiliaji Bw. Amani Mafuru wakati akitoa taarifa ya wiki ya maji mkoani Irinaga leo, Kushoto ni Naibu Waziri wa maji Mh. Grayson Rwenge.
 Rais Jakaya Kikwete akisikiliza maelezo ya Mkurugenzi wa maji Mijini Wizara ya Maji na Umwagiliani Bw.Yohana Monjesa katika kilele cha wiki ya maji mkoani Iringa.
Mtaalam wa Maendeleo ya Jamii katika mradi wa wa Mazingira katika Ziwa Victoria BwRaymond Mariki akitoa maelezo ya utekelezaji wa majukumu ya mradi huo mbele ya Rais Jakaya Kikwete katika maonyesho ya wiki ya maji Mkoani Iringa yaliyomalizika leo.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wakuu na na wafadhili (mstari wa mbele) sambamba na kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya wiki ya maji Kitaifa yalifikia tamati leo na kufungwa rasmi na Rais Kikwete mapema leo jioni kwenye Uwanja wa Samora mkoani Iringa.

Rais Jakaya Kikwete akikabidhi cheti cha shukrani kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) na Kupokelewa na Mkurugenzi wake wa Mahusiano na Mawasiliano Teddy Mapunda. Pia SBL walipokea Cheti cha ushiriki wa maonesho hayo. 
 Baadhi ya viongozi  wa Serikali na wageni waalikwa wakiwa ameketi jukwaa kuu
Rais Kikwete akielekea kukagua Mabanda ya maonesho ndani ya Uwanja wa Samora mapema jioni hii,ambapo Rais Jakaya Kikwete leo amefunga Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kitaifa Mkoani Iringa. Pamoja na kuhutubia katika kilele hicho pia Rais alipata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ya watoa huduma za maji na wadau mbalimbali wa maji nchini.
Pichani ni Rais Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Bi Teddy Mapunda mara baada ya kulitembelea banda hilo,ambao ndio wadhamini wakuu wa maadhimisho hayo ya mwaka huu yaliyofanyika uwanja wa Samora Mjini Iringa. na pichani kati ni Meneja Miradi Endelevu na Uwajibikaji wa SBL, Nandi Mwiyombela.
Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Bi Teddy Mapunda akitoa maelezo mafupi kwa Mgeni rasmi,Mh Rais Kikwete  mara baada ya kulitembelea banda hilo.

Thursday 22 March 2012

WASHINDI WA PROMOSHENI YA AIRTEL MZUKA ARUSHA WAKABIDHIWA ZAWADI ZAO.

Afisa masoko wa Airtel kanda ya kaskazini Geofrey Sayore akikabidhi simu ya Samsung GT 3210 kwa mshindi wa promosheini ya Mzuka wa Airtel bwn festo Ronald Msoffe wa Arusha mara baada ya kutangazwa kuwa moja kati ya washindi wa promosheni hiyo inayoendea na wateja wa Airtel kujishindi zawadi mbalimbali zikiwemo Simu, ipad, muda wa maongezi na pesa taslimu.