Monday 27 October 2014

Wanaokiuka kutoa taarifa waonywa


NA RACHEL KYALA
KIONGOZI yeyote atakayeshindwa kurejesha fomu za tamko la Rasilimali na Madeni ya Viongozi katika muda uliowekwa, anapaswa kutambua kuwa hilo ni kosa na ukiukwaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma, imeelezwa.
Taarifa kwa Umma iliyotolewa na Kamishna wa Maadili, imesema  viongozi wa umma wanapaswa kujua kuwa si wajibu wa kisheria kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi kuwapelekea viongozi fomu hizo.
Aidha kupitia taarifa hiyo wametakiwa kuzingatia kuwa ni wajibu wa kiongozi husika kuzitafuta kwa wakati ili kutekeleza matakwa hayo ya kisheria.
Taarifa hiyo inasema fomu hizo tayari zimeanza kutolewa na zinapatikana katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Dar es Salaam na katika ofisi za kanda zilizoko Kibaha, Arusha, Dodoma, Tabora, Mwanza, Mbeya na Mtwara. 
Kamishna wa Maadili kupitia taarifa hiyo alisema kiongozi atakayeshindwa kurejesha kwa tarehe husika atachukuliwa hatua kama ambavyo kifungu cha 15 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995 kinavyoeleza.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru