Sunday 17 May 2015

Kocha Newcastle alia na kiwango




KOCHA Mkuu wa Newcastle John Carver, amesema amesikitishwa na kiwango kilichoonyeshwa na timu yake katika mchezo wa Ligi Kuu England.Katika mchezo huo, Newcastle ilipokea kipigo cha mabao 2-1, dhidi ya QPR.Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Carver alisema timu ilipoteza mchezo huo baada ya kucheza chini ya kiwango.

Carver alisema timu yake ingeweza kushinda lakini safu ya ulinzi ilimuangusha baada ya kukosa umakini na kuruhusu wapinzani wao kupenya na kupata mabao.

"Timu yangu ilicheza chini ya kiwango hali ambayo imesababisha kupoteza mchezo wetu dhidi ya QPL lakini matokeo hayo hayatatukatisha tamaa," alisema Carver.

Kutokana na matokeo hayo, Newcastle inashika nafasi ya nne kutoka mkiani baada ya kujikusanyia pointi 34 wakati QPR ipo nafasi ya pili mkiani ikiwa na pointi 30.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru