Thursday 2 January 2014

Polisi mgodi wa Resolute kuchunguzwa


Na Chibura Makorongo, Nzega
POLISI mkoani Tabora, wamesema watafanya uchunguzi kuwabaini askari wake wanaolinda eneo la mgodi wa Resolute, ambao wanadaiwa kuchukua rushwa kisha kuwaruhusu wavamizi kuingia katika eneo linalochimbwa dhahabu.
Wachimbaji wadogo waliotimuliwa eneo la Kijiji cha Mwanshina ambalo linadaiwa kumilikiwa na mgodi huo, walimweleza Mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kigwangala na viongozi wengine kuwa polisi walikuwa wakiwaomba rushwa.
Malalamiko hayo yalitolewa kwenye mkutano wa hadhara mbele ya Dk. Kigwangala, ambapo walisema pamoja na kufukuzwa, lakini polisi huchukua rushwa ya mpaka sh. milioni tatu, kisha huwaruhusu watu kuingia ndani ya eneo la mgodi na kuchimba dhahabu usiku.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Peter Ouma, alisema wanajipanga kuanza kuchunguza tuhuma hizo na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.
“Nimesikia malalamiko ya wachimbaji kuwa Polisi wetu wanaolinda eneo la mgodi hupokea fedha kutoka kwa baadhi ya matajiri na kuwaruhusu kuchimba dhahabu usiku,’’ alisema.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru