Wednesday 3 September 2014

Afa kwa kuangukiwa na ukuta wa kanisa


NA RACHEL KYALA
M Grace Zephaniah (9), mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwenge, wilayani Kinondoni, amefariki dunia baada ya kuangukiwa na ukuta wa Kanisa la Calvary, lililoko Mlalakuwa, Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alisema kifo hicho kilitokea juzi saa 1.30 usiku. Hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala kwa uchunguzi zaidi huku upelelezi ukiendelea.
Wakati huo huo, mtu mmoja ambaye hakufahamika jina, alifariki dunia jana saa 6.30 usiku, baada ya kutumbukia katika Bahari ya Hindi, maeneo ya Ferry, Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, Kihenya wa Kihenya, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa marehemu anakadiriwa kuwa  na umri wa kati ya miaka 40 hadi 45.
Kamanda Kihenya alisema mwili wa mahehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Vijibweni.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru