‘Fanyeni uamuzi sahihi
uchaguzi mkuu Oktoba’
WAKATI Taifa likielekea katika uchaguzi
mkuu wa rais, wabunge na madiwani, Watanzania wametakiwa kufanya uamuzi sahihi,
ili kuwapata viongozi watakaowaletea maendeleo.
Pia wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha
katika katika daftari la kudumu la wapigakura, ili watumie haki yao ya kikatiba
kuwachagua viongozi wanaowataka.
Wito huo ulitolewa juzi na Askofu wa
Jimbo la Shinyanga, Liberatus Sangu,
katika sherehe ya Jubilee ya miaka 55 ya Padri Paul Fagani, wa Parokia ya Kanisa Katoliki la Mt. Petro Songambele Nkololo, wilayani Bariadi,
mkoani Simiyu, iliyofanyikia kanisani hapo.
Askofu Sangu alisema katika kipindi hiki,
Watanzania hawana budi kuchunguza kwa makini na kufanya uamuzi sahihi, ili
kuwapata viongozi watakaotumikia taifa kwa uadilifu na weledi.
Mbali na hilo, askofu huyo aliwataka waumini wa dini hiyo kupiga vita mauji
ya vikongwe pamoja na watu wenye ulemavu wa ngozi, huku akibainisha kuwa dini
hiyo haikubalini na jambo la binadamu kumtoa roho mwenzake.
Katika Jubilee hiyo iliyohudhuriwa na
mamia ya wakazi wa Wilaya ya Bariadi, Padri Paul Fagani, alihitimiza miaka 55 ya upadri, tangu alipopata daraja
hilo nchini Marekani, ambapo mwaka 1960 alikuja Tanzania na kuanzishwa Parokia ya Buhangija Shinganya kama Paroko Msaidizi
na mwaka 2007 alianzisha Parokia hiyo ya Mtakatifu. Petro Songambele Nkololo.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Toa Maoni Yako Kwa Uhuru