Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Thursday 26 September 2013

Warioba: Katiba mpya haitaletwa kwa vurugu


Rabia Bakari na Mohammed Issa

TUME ya Mabadiliko ya Katiba, imeonya kauli na vitendo vya wanasiasa vinavyoendelea kuhusu mchakato wa kupata katiba mpya vinaweza kusababisha madhara na kuligawa taifa vipande.
Pia, imesema kuwa Katiba haiwezi kupatikana kwa maneno ya majukwaani, maandamano au vikundi kuzunguka nchi nzima na kwamba, msingi imara ni kutumia busara ya mazungumzo na maridhiano.
Mbali na hilo, imetahadharisha iwapo Katiba mpya ambayo mchakato wake unaendelea kwa sasa nchini itapatikana kwa mapambano, basi  hakutokuwa na umoja wala mshikamano wa kitaifa miongoni mwa Watanzania.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ambapo alisema baadhi ya wanasiasa wanaingilia mchakato huo kwa manufaa binafsi na ndio sababu kelele haziishi kwenye majukwaa.
Vyama vitatu vya upinzani kwa sasa vipo kwenye kile kinachodai kufanya ziara nchi nzima kupinga Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kwa madai kuna vipengele vimechomekewa.
Wabunge wa vyama hivyo wakiongozwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, walisusia kikao cha Bunge kupitisha muswada huo, ambapo baadaye ilibainika kuwa mambo waliyotarajia kuyapenyeza hayakufanikiwa.
Pia, taarifa zinaeleza vyama hivyo vimekuwa kwenye mikakati kamambe ya kuhakikisha vinavuruga mchakato huo kwa maslahi yao binafsi, huku baadhi ya wafadhili wakiwa nyuma.
"Vyama vingi vya siasa vimejitazama vyenyewe, nia yetu ni kupata katiba ya wananchi wote... hatuko kwenye mashindano wala misuguano.
"Tunajenga, hatuko kwa ajili ya kubomoa... tunahitaji katiba itakayoheshimika na Watanzania wote na itakayokuwa chachu ya maendeleo," alisema Jaji Warioba na kuongeza kuwa.
"Kinachofanywa sasa na baadhi ya wanasiasa kinaweza kuleta madhara makubwa na kuwagawa Watanzania, hivyo kuiweka nchi katika wakati mgumu.
Jaji Warioba alisema kama kuna sehemu ambayo  wanasiasa wanadhani wametofautiana ni vyema kutafakari kwa pamoja kwa kukaa chini kwa lengo la kutafuta ufumbuzi na si kutumia majukwaa, jambo ambalo ni hatari na haliwezi kuwa na tija.
Alisema Katiba inayotafutwa ni ya Watanzania na sio kwa ajili ya vikundi vya watu, na kwamba umefika wakati kwa Watanzania kuungana na kutokubali kuyumbishwa.
Jaji Warioba alisema katiba itapatikana kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria na si maneno ya majukwaani.
Alisema tume hiyo sio msimamizi wa sheria, na kwamba inafanya kazi kwa kufuata taratibu za kisheria, zilizopitishwa na Bunge wakati wanakabidhiwa jukumu hilo.
Aliongeza kuwa baadhi ya vyama vya siasa wakati wa kupitia maoni ya kuboresha rasimu havikufuata utaratibu uliowekwa na vilitumia mihadhara kunadi matakwa yao.
Alisema wajumbe wa tume hiyo, walipata wakati mgumu na wengine walivurugwa kiakili kutokana na matamshi ya viongozi wa kisiasa walioamua kuvuruga utaratibu wa kukusanya mapendekezo ya rasimu.
Jaji Warioba alisema tume iliruhusu taasisi, asasi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana kuunda na kuendesha Mabaraza ya Katiba kwa lengo la kujadili na kuitolea maoni Rasimu ya Katiba Mpya.
Hata hivyo, alisema baadhi ya vyama vya siasa viliingilia uhuru wa wajumbe katika kutoa maoni na kuna maeneo mengine wajumbe wa mabaraza walifundishwa mambo ya kuzungumza.
Kwa mujibu wa Jaji Warioba, katika baadhi ya mikutano, wajumbe wa mabaraza waliwajadili wawakilishi kutoka tume, badala ya kuijadili rasimu ya katiba iliyotolewa.
Alisema pamoja na changamoto hizo, tume imetekeleza majukumu yake kwa kiasi kikubwa na hivi sasa wanachambua maoni, ili yaingie kwenye rasimu ya pili, ambayo itawasilishwa kwenye Bunge la Katiba.
Jaji Warioba alitumia fursa hiyo kukanusha taarifa kuwa kuna wajumbe wa Tume wamejiuzulu, ambapo alisema wajumbe wote wanaendelea na kazi waliyopewa na kwamba, hakuna aliyetishia kujiuzulu kama ilivyodaiwa.







Mtanzania mwingine afa na dawa za kulevya

Na Mwandishi Wetu
MTANZANIA Moza Gaza (25), amefariki dunia baada ya kutumia dawa za kulevya aina ya Cocaine aliyokuwa amechanganya na pombe kali.
Moza amefikwa na umauti ikiwa ni siku tatu, baada ya mfanyabiashara Rajabu Rajabu mkazi wa Ilala, kufariki dunia baada ya pipi 33 za Heroine kumpasukia tumboni.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na polisi wa India, marehemu Moza na rafiki yake wa kiume ambaye hajafahamika, walikwenda kwenye sherehe iliyohudhuriwa na Wanaigeria.
Polisi walisema sherehe hiyo ilifanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Stallion, katika eneo la Safdarjung Enclave, karibu na soko la Green Park Kusini mwa Delhi.
Taarifa hiyo ilisema Moza alikuwa anaishi na rafiki yake huyo ambaye hajafahamika katika eneo la South Extension II, na kwamba alianguka kwenye sherehe hiyo baada ya dawa alizokuwa amemeza kumzidi.
Hata hivyo, polisi walisema marehemu Moza alikimbizwa katika hospitali ya Sukhmani, na alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika hospitali hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya polisi wa India, ripoti za kitabibu na maelezo kutoka kwa mashuhuda, marehemu alifariki baada ya kuchanganya dawa na pombe.
Polisi wamesema wanamshikilia meneja wa hoteli hiyo, msaidizi wake na rafiki wa kiume wa marehemu huyo kwa mahojiano na wanaendelea kumtafuta aliyeandaa sherehe hiyo.
Walisema wamefanya mawasiliano na ubalozi wa Tanzania uliopo India ili kuwataarifu ndugu zake kuhusiana na kifo cha Moza.
Mkuu wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) Tawi la Tanzania, Gustav Babile, alisema hawajapata taarifa la tukio hilo na kwamba watalifuatilia.
Naye, Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Kudhibiti Dawa za Kulevya wa Jeshi la Polisi, Godfrey Nzowa, alisema hawana uhakika wa tukio hilo, na kwamba wanalifuatilia kwa karibu.
“Hili tukio bado hatujalipata kikamilifu, lakini tunalifanyia kazi ili tuweze kuelewa undani wake,” alisema.
Kwa mujibu wa Nzowa, wananchi wa India wameruhusiwa kulima Heroine kwa ajili ya matumizi ya dawa mbalimbali za kitabibu.
Hata hivyo, alisema baadhi ya wafanyabiashara, wameanza kuingiza viashiria vya dawa hizo hapa nchini kinyume cha sheria.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mkumbwa Ali, hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake ya mkononi kutokuwa hewani.

Agizo la Pinda laanza kutekelezwa



NA SHAABAN MDOE, NGORONGORO
AGIZO la Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), kuigawia chakula cha bure jamii ya watu wa Kimasai wapatao 87,000, limeanza kutekelezwa.
Hatua hiyo inayotokana na mamlaka hiyo jana kuanza kugawa kiasi cha tani 700 za mahindi ya chakula kwa jamii hiyo.
Mgawo huo ulianza kutekelezwa ukianzia kata ya Olbalibali, ambapo kaya 1,000 za vitongoji vitano vya tarafa ya Ngorongoro zilipokea chakula hicho kilichogawiwa katika kijiji cha Meshili, huku kaya 508 zikisubiri awamu ijayo.
Vitongoji vilivyopata chakula hicho ni Ngurman, Lorkujita, Nibojijita, Ildonyogoli na Meshili, ambapo kila kaya ilipata debe moja la mahindi bure.
Chakula hicho kilikuwa kimehifadhiwa kwenye maghala, huku kila kaya ikiendelea kusubiri kugawiwa kiasi kingine cha magunia 10.
Akizungumzia mpango huo, Ofisa Ugani wa NCAA, Francis Kone alisema hadi sasa wamenunua magunia 29,000 ya mahindi kutoka wilayani Karatu kwa ajili ya mpango huo wa ili kuwawezesha kuondokana na tatizo la njaa.
Awali, alisema kabla ya agizo hilo, walikuwa na mpango wa kugawa chakula hicho kwa awamu tatu, ya kwanza wakipanga kununua magunia 900, pili magunia 10,000 na tatu magunia 10,000, lakini baada ya agizo hilo, wamelazimika kununuaa magunia yote kwa mkupuo.
Hata hivyo, alisema mamlaka hiyo imedhamiria kutoa magunia mengine 36,000 ya mahindi kwa jamii hiyo, mbali na chakula kilichoahidiwa na Pinda cha magunia matano kwa awamu ya kwanza kwa kila kaya na mengine matano kwa wamu ya pili.
Kone alisema hatua hiyo inatokana na kutambua kuwa hadi sasa chakula kinachogawiwa ni kwa kaya zile zisizo na uwezo kabisa wa kupata chakula.
Mwanakijiji Kanunga Marau aliishukuru serikali kwa chakula hicho, lakini aliiomba kutochelewesha mgawo wa magunia 10 kwa kila kaya ili kuwawezesha wananchi kuwa na uhakika wa chakula wakati wote.
Alisema serikali isiwasahau kwa kuamini chakula kilichotolewa kitakidhi, hasa ikizingatia sheria za uhifadhi katika eneo hilo haziwaruhusu kuendesha hata kilimo cha kujikimu.
Diwani wa Kata hiyo, Metui Ole Shaudo aliipongeza serikali kwa niaba ya wananchi na kusisitiza bado mahitaji ya chakula katika kata yake ni makubwa, hasa ikizingatiwa kaya nyingi ni zile zisizo na uwezo kabisa wa kujipatia chakula.
Aliiomba serikali kutimiza ahadi ya ugawaji wa magunia 10 kwa awamu mbili kwa kila kaya ili kuwajengea imani na kuwafanya waendelee kuwa wahifadhi waaminifu wa hifadhi hiyo na wanyamapori waliopo.
Mwanzoni mwa juma lililopita, Waziri Mkuu Pinda akiwa katika tarafa hiyo aliwaahidi wananchi hao kuwa serikali itabeba jukumu la kuwapatiwa chakula wananchi hao kila mwaka wakati ombi lao la kutaka waruhusiwe kuendesha kilimo likifanyiwa kazi.
Ends.

CCM YATIKISA RORYA


MAELFU ya wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Chama hicho Abdulrahaman Kinana, alipokuwa akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Shirati Obwere wilayani Rorya, jana. 

Wednesday 25 September 2013

KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika juzi, Wilayani Rorya, mkoani Mara. (Picha na Adam Mzee).

Kinana arusha kombora zito


NA WAANDISHI WETU
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimevitaka vyama vya upinzani kutotafuta umaarufu kupitia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya CCM.
Pia, kimesema kinatekeleza miradi mbalimbali kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi wote bila kujali itikadi za vyama.
Wakati CCM kikiendelea kung’ara katika kuwahudumia wananchi, CHADEMA kinazidi kumeguka, ambapo wilayani Handeni kimefutika baada ya wanachama zaidi ya 300 kukihama na kujiunga na CCM, wakiwemo viongozi wake.
Hayo yalijitokeza juzi wakati ya ziara ya Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Taifa, Abdallah Bulembo, ambapo viongozi na wanachama walikabidhi kadi zao CCM.
Mbali na hilo, Chama kimewataka viongozi wote kuanzia ngazi ya shina hadi taifa kuacha utendaji wa mazoea na kuwa wakali na kuisimamia serikali katika utekelezaji shughuli za maendeleo.
Msiamamo huo ulitolewa jana Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, mjini Musoma, wakati akiwahutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo.
Alisema wapinzani wanapaswa kuacha kimbelembele na kujinasibisha kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayofanywa na serikali iliyo chini ya CCM kwa kuwa, iko kwenye Ilani na ahadi za Chama kwa wananchi na taifa kwa jumla.
Kinana alitoa mfano wa mradi mkubwa wa maji ya Ziwa Victoria unaoendelea kujengwa mjini Musoma, ambapo alisema licha ya wapinzani kudai ni wao, lakini ukweli ni kwamba mradi huo ni ahadi ya CCM na sasa inautekeleza.
“Wakati wenzetu wa upinzani wakipita wakidanganya wananchi na kujinasibisha na miradi yetu ya maendeleo, sisi tutaendelea kuitekeleza kwa maslahi ya Watanzania wote,” alisema.
Mbali na mradi huo serikali mkoani Mara, pia inaendelea na ujenzi wa Hospitali ya Rufani ya Kwangwa, inayojengwa wilayani Musoma.
Mapema, akiwahutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Shirati wilayani Rorya mkoa wa Mara, Kinana alisema sasa ni wakati kwa wana-CCM kuhakikisha wanakuwa wakali na kuisimamia serikali ili itimize majukumu yake kwa Watanzania.
“Nawaagiza wana-CCM wote kuanzia ngazi ya shina, tawi, kata, wilaya mkoa hadi taifa kuwa wakali na kuibana serikali kuhakikisha inatimiza majukumu yake kwa taifa. Bila kufanya hivyo siku moja itakula kwetu,” alisema.
Kinana alisema serikali ya CCM imefanya mambo mengi kwa Watanzania na kuahidi kuwatumikia kadri iwezekanavyo, hivyo wananchi wanapaswa kuwa makini kutokana na kauli za wapinzani.
Akizungumzia miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo, alisema ndani ya mwaka huu wa fedha serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali.
Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na ile ya kusambaza umeme na maji vijijini, ambapo jumla ya vijiji 30 vitanufaika.
Alisema, mbali na miradi hiyo, serikali pia inaendelea na ujenzi wa malambo mawili ya maji katika kata ya Utegi wilayani humo.
Kwa upande wake, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, aliwataka wananchi wa Shirati na Rorya, hususan vijana kutokubali kushawishika na propaganda za wapinzani kuhusu katiba mpya zenye lengo la kuibua mtafaruku katika jamii.
Nape alisema hakuna chama chochote cha siasa kilicho na kauli ya mwisho kuhusu suala hilo, bali wananchi ndio watakaoamua ni aina gani ya katiba wanayoihitaji.
Kwa mujibu wa Nape, viko baadhi ya vyama vya siasa vilivyodai kuungana na kupita mikoani kwa ajili ya suala la katiba mpya, Watanzania wanapaswa kuwa makini na yale watakayoelezwa na watu hao endapo yatakuwa yakiashiria uvunjifu wa amani.
Kinana na Nape wamehitimishisha ziara yao ya kikazi ya wiki tatu katika mikoa mitatu ya Kanda ya Ziwa ya Shinyanga, Simiyu na Mara.
Kutoka Handeni, Mwandishi Wetu anaripoti kuwa, Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Taifa, Abdallah Bulembo, ameisambaratisha kambi ya CHADEMA baada ya ëkukombaí wanachama 380 wa chama hicho, ukiwemo uongozi wa juu wa wilaya.
Uamuzi wa viongozi na wanachama hao kujiunga na CCM, umeelezwa kuwa wa kihistoria kwa chama hicho wilayani humo tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi.
Wanachama na viongozi hao walichukua uamuzi huo baada ya kukabidhi kwa Bulembo kadi zao za uanachama na nyaraka zote muhimu za kuendeshea ofisi ya wilaya hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliyofanyika juzi katika Kata ya Kwamatuku.
Viongozi hao ni pamoja na Mwenyekiti wa Wilaya hiyo, Luka Selemani, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Maguruwe, Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya Wilaya.
Wengine ni Katibu wa wilaya hiyo Athumani Ngido, ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya Wilaya na Mkoa wa Tanga, Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Wilaya hiyo, Jackson Francis, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kata ya Kabuku Nje na aliwahi kuwa mgombea udiwani katika uchaguzi mkuu uliopita.
Mbali na hao, wamo Mwenyekiti wa BAVICHA tawi la Kwamatuku, Abraham Mtengwa na mjumbe wa kushughulikia migomo ya chama hicho Juma Mkomba.
Akihutubia wananchi katika mkutano huo wa hadhara, Bulembo alisema kukimbia kwa viongozi na wanachama hao ni ishara kuu ya chama hicho kusambaratika katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.
Alisema kadri siku zinavyoenda, CHADEMA itazidi kusambaratika kutokana na baadhi ya viongozi wake kukumbatia madaraka, huku wengine wakiachwa kuwa wapigadebe tu.
ìDhambi ya umimi, udugu na urafiki utaimaliza CHADEMA, kwani kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kubaki ndani ya CHADEMA akitazama wanandugu wakigawana vyeo.
ìMaana yake nini... kama huna baba, mama au mjomba huwezi kupata cheo ndani ya CHADEMA na ili kuamini hilo angalieni wabunge wao wa viti maalumu jinsi walivyoteuliwa ëkiudugu na kiushikajií,î alisema Bulembo.
Alisema wabunge hao wa viti maalumu hawakuteuliwa kulingana na matokeo ya ushindi iliyoupata CHADEMA katika mikoa mbalimbali, bali umelenga maeneo wanakotoka viongozi wakuu wa chama hicho.
Kwa upande wake aliyekuwa Katibu wa wilaya hiyo, Ngindo, alisema kuhama kwao katika chama hicho ni pigo kwa CHADEMA.
Ngindo alisema waliamua kufanya uamuzi mgumu wa kukihama chama hicho kutokana viongozi wake wa juu kujithamini wenyewe bila kujali wengine waliopo katika wilaya.
ìHiki si chama, bali ni kampuni inayojiendesha kwa kujali maslahi binafsi. Kama kingekuwa chama cha siasa, basi hivi sasa tungekuwa mbali, hususan katika wilaya hii,î alisema.
Naye Selemani aliyekuwa Mwenyekiti wa Wilaya hiyo, alisema kuanzia sasa watapanga mikakati ya kukifuta chama hicho ili kisisikike katika wilaya hiyo.
ìHandeni unapoitaja CHADEMA maana yake unataja kikosi hiki kilichorudi leo CCMÖ sasa kazi moja tu kuhakikisha kila mtu aliyekuwa CHADEMA anarudi CCM kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa hapo mwakani,î alisema.

Maiti ya dawa za kulevya Mazito yafichuka


Na Mwandishi Wetu
SIRI ya kifo cha mfanyabiashara Rajabu Rajabu aliyefariki dunia, baada ya kumeza pipi 33 za dawa za kulevya zenye thamani ya mamilioni ya fedha, imefichuka.
Marehemu Rajabu mkazi wa Ilala, Dar es Salaam, alifariki dunia juzi, baada ya dawa hizo aina ya Heroine kumpasukia tumboni.
Kufuatia tukio hilo, Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, inawashikilia asri Rajabu ‘Robot’ na Mwanaisha Kapama, wakazi wa Kigogo Luhanga, wakiwa na maiti ya mfanyabiashara huyo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umeibua siri nzito baada ya kubaini kuwa kabla ya umauti kumfika, marehemu aliondoka na dawa hizo kutoka Dar es Salaam kwenda Msumbiji.
Habari za uhakika kutoka chanzo chetu cha habari zinadai kuwa, marehemu alifikia katika nyumba ya kulala wageni mkoani Mtwara kwa ajili ya kuangalia hali ya usalama katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji.
Chanzo hicho kilidai marehemu alikaa katika nyumba hiyo kwa muda wa siku tatu na kwamba, afya yake ilibadilika ghafla na kushindwa kutoka nje ya nyumba hiyo.
“Huyo marehemu alikodi chumba kwenye ‘Guest’ moja ili kuangalia hali ya usalama mpakani ili aweze kuendelea na safari yake.
“Lakini hafla hali yake ilibadilika na kukaa ndani siku nzima bila kutoka nje, hivyo mhudumu wa ile nyumba alilazimika kuingia ndani ya chumba kumuangalia.
“Hata hivyo, mhudumu alimuona akiwa katika hali mbaya na ndipo alipomwuliza wenyeji wake na alimpa namba ya simu ya kaka yake anayeishi Ilala,” kilisema chanzo hicho.
Kwa mujibu wa chanzo chetu hicho, baada ya kaka wa marehemu kupewa taarifa ya mdogo wake kuumwa, walilazimika kwenda Mtwara na mke wa marehemu.
Kilisema kaka wa marehemu aliondoka na gari aina ya Toyota Land Cruiser VX na kwamba, marehemu alikuwa amepakatwa na mke kwenye kiti cha nyuma ya gari hiyo.
Chanzo hicho kilisema kuwa, wakati wanarudi walipofika maeneo ya TAZARA, Dar es Salaam, Rajabu alifariki dunia na dereva wa gari hilo aliteremka kwa muda.
“Huyu jamaa alifia pale TAZARA na alikuwa amepakatwa na mkewe… baada ya kubaini amefariki ilibidi dereva ateremke kidogo kuhakikisha kama ni kweli.
“Wananchi baada ya kumwona dereva ameteremka kwenye gari na kuja nyuma, ndipo walipoitilia shaka na kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Buguruni, ambapo polisi walianza kufuatilia ile gari,” kilieleza chanzo hicho.
Kilisema marehemu alipelekwa maeneo ya Tabata Mawenzi na muda mfupi baada ya kuingizwa kwenye nyumba hiyo, askari walifika na ndipo alipobainika alikuwa amemeza dawa.
Chanzo chetu hicho cha habari kilisema kuwa, marehemu anajihusisha na biashara hiyo kwa muda mrefu kwenye nchi mbalimbali, ikiwemo Msumbiji.
Juzi, gazeti hili liliripoti habari ya kufariki kwa mfanyabiashara huyo, baada ya kuwa amemeza pipi 33 za dawa za kulevya, ambazo hata hivyo, zilimpasukia tumboni.
Siku moja baada ya kuripoti habari hiyo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova alisema wanawashikilia Rajabu na Mwanaisha wakiwa na maiti ya marehemu.
Kova alisema taarifa zinaonyesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa usafirishaji wa dawa za kulevya, na kwamba kabla ya kurudi nchini alikuwa anatumikia kifungo barani Asia.
Alisema baada ya polisi kupata taarifa ya tukio hilo, walikwenda nyumbani kwa Rajabu maeneo ya Tabata na kumhoji, ambapo waligundua uwepo wa maiti sebuleni ikiwa imelazwa chali kwenye godoro.
Kova alisema Rajabu ndiye mmiliki wa chumba ilimokutwa maiti na uchunguzi unaonyesha marehemu alifika kutoka Mtwara, na juzi na kabla ya kufa mfanyabiashara huyo, alikwenda bafuni kuoga na alirudi katika chumba hicho na ndipo alipokutwa na umauti.
Kamishna huyo, alisema mazingira ya kifo hicho ndiyo yaliyosababisha polisi kupata taarifa na walipofika eneo la tukio waliuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi.
Hata hivyo, alisema uchunguzi unaendelea
ili kubaini mtandao wa usafirishaji wa dawa hizo ambao umehusisha marehemu na watakaokamatwa watachukuliwa hatua za kisheria.

Babu wa Loliondo aibuka ‘kivingine’


Na Mwandishi Wetu
MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapila, amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonyesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na baadaye kioo cha dunia.
Alitoa kauli hiyo juzi asubuhi, mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia, akiwa njiani kurejea mjini Arusha.
Mchungaji huyo mstaafu maarufu ‘Babu wa Samunge’, alisema kuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia, lakini hayakutokea Israel, lakini sasa yatafanyika Samunge.
“Mungu ametupenda mno, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nitayaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea,” alisema huku akishangiliwa.
Alisema katika ufunuo aliopewa na Mungu, ameonyeshwa kwamba watu wengi zaidi watafurika kijijini Samunge kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Alitumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa misaada iliyotoa wakati wa ‘kugawa kikombe’, ikiwemo mahema, maji na ulinzi.
Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Arusha kwa ziara maalumu ya kusikiliza matatizo ya ardhi yanayowakabili wakazi wa wilaya ya Ngorongoro, katika tarafa za Ngorongoro, Loliondo na Sale, alisema anakubaliana na utabiri wa Mchungaji Mwaisapila.
Pinda akithibitisha kuhusu ubashiri wa babu huyo, alisema Tanzania ni nchi iliyojaliwa gesi na mafuta mengi ambavyo vitabadili sura ya nchi.
“Mungu ametupa gesi nyingi mno, katika miaka miwili tutakuwa na umeme kila mahali. Tuna makaa ya mawe ambayo ni nishati kubwa na sasa tuna fursa ya kupata nishati ya umeme kutoka ardhini katika Ziwa Natron,” alisema.
Waziri Mkuu alisema Tanzania imekuwa kimbilio la kila mwekezaji, na kuongeza kwamba sababu kubwa ni amani na utulivu uliopo nchini.
Aliwaeleza wakazi wa Samunge kwamba, mwakani mkandarasi wa barabara atakuwa katika eneo lao kwa ajili ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, ambapo awamu ya kwanza itaanzia Wasso hadi Mto wa Mbu kupitia Samunge.
Akitoa ombi maalumu kwa ajili ya vijana mbele ya Waziri Mkuu, Elias Kalumbwa, alisema wanaiomba serikali iwachimbie bwawa ili waweze kujiajiri kupitia kilimo cha mboga na matunda.
Hata hivyo, Kalumbwa ambaye amesomea masuala ya wanyamapori, alisema eneo hilo liko katika mto wa msimu unaopita kijijini hapo.
“Eneo la kuchimba bwawa liko katika mto wetu, vijana tunaweza kujiajiri, endapo tutapata bwawa ili tufanye kilimo cha umwagiliaji,” alisema huku akishangiliwa.
Naye Bibi Martha Sereri (70) alimweleza Waziri Mkuu kwamba, wanaomba jimbo la Ngorongoro ligawanywe kwa sababu ni kubwa kiasi kwamba inamuwia vigumu mbunge wao kufika maeneo yote.
Pia, bibi huyo aliomba wapatiwe walimu wa masomo ya sayansi na hisabati kwa ajili ya shule 10 za sekondari zilizoko kwenye tarafa yao.
Aidha, alimwomba Waziri Mkuu awaweazeshe kupatiwa mikopo kwa ajili ya ununizi wa matreka ili waweze kuongeza ukubwa wa mashamba yao.
“Tunaomba mikopo ya matrekta na plau, haya mashamba umeyaona njiani yamelimwa na Wakenya. Ukikodisha trekta kila ekari ni sh. 100,000. Je tutafika wapi? Mkitukopesha matrekta mtakuwa mmetusaidia zaidi,” alisema.
Akijibu hoja hizo, Waziri Mkuu alisema hoja zao ni za msingi na kwamba, suala la vijana kupatiwa bwawa inawezekana kupitia Mpango wa Maendeleo ya Kilimo wa Wilaya (DADP).
“Andaeni andiko lenu, inabidi litoke kwa wananchi na siyo serikalini. Mkituletea ni jambo linalowezekana, kwani liko ndani ya mipango ya wilaya.”
Kuhusu ukubwa wa jimbo, Waziri Mkuu aliwaambia wakazi hao kwamba inawezekana kuongeza jimbo isiwe suluhisho la matatizo yao kwa sababu ya jiografia ya eneo lao.
“Kuongeza jimbo inaweza isiwe jibu la kila kitu, kwani matatizo mnayopata yanatokana na jiografia ya eneo lenu, kutoka Ngorongoro, Loliondo hadi huku Sale. Mimi nadhani tuangalie uwezekano wa kuwapa halmashauri ili kusogeza huduma kwa wananchi. Tutaangalia njia zote mbili na kuona ipi italeta majibu ya haraka kwenu,” alisema.

Madereva kupimwa afya zao


Na Latifa Ganzel, Morogoro
SERIKALI imesisitiza mpango wa upimaji wa afya za madereva kwenda sambamba na ukaguzi wa magari ili kupunguza ajali za barabarani.
Alisema kwa kufanya hivyo, kutawahakikishia wananchi
usalama wao na mali zao.
Mkuu wa Wilaya, Saidi Amanzi, alisema hayo wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabara, ambayo inakwenda sambamba na upimaji wa afya kwa madereva katika maeneo ya Mikese mkoani hapa na Msoga, Pwani.
Kaulimbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni “Usalama barabarani inaanza kwangu, kwako na sisi sote.”
Amanzi alisema roho za abiria na mali ziko mikononi mwa madereva, hivyo hawana budi kutambua dhamana waliyonayo.
Kutokana na hilo, alikiagiza kikosi cha usalama barabarani kuhakikisha upimaji kama huo wa afya unakwenda sambamba na ukaguzi wa magari ili kupunguza ajali.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, aliwaasa madereva kuzingatia upimaji wa afya zao kutokana na dhamana waliyonayo ya kubeba watu, mali na mizigo yenye thamani kubwa.
Naye Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa, Boniface Mbao, alisema ni vyema madereva wakajenga tabia ya kupima afya zao kwa hiyari kwa manufaa yao.
Naye, Mwanasheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), iliyodhamini shughuli hiyo, Steven Kilindo, aliahidi kushirikiana na kikosi hicho kuhakikisha ajali zinapungua kama si kumalizika kabisa.
Mpango huo pia unashirikisha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro na Tungi Kibaha, ikiwa imelenga kuwafikia madereva 1,300 watakaopita barabara kuu za mikoa ya Morogoro na Pwani.
Ends.

Tuesday 24 September 2013

Polisi yanasa maiti yenye dawa za kulevya

Na Mwandishi Wetu
POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, inawashikilia Nasri Rajabu ëRobotí na Mwanaisha Kapama, wakazi wa Kigogo Luhanga, wakiwa na maiti ya mfanyabiashara Rajabu Rajabu ikiwa na dawa za kulevya.
Watuhumiwa hao wamekamatwa siku moja baada ya gazeti hili kuripoti habari ya kufariki kwa mfanyabiashara huyo, baada ya pipi 33 za dawa za kulevya alizokuwa amezimeza, kumpasukia tumboni.
Kufa kwa Rajabu kumeibua mambo mazito, baada ya polisi kudai taarifa zinaonyesha kuwa, alikuwa mhalifu mzoefu wa usafirishaji wa dawa za kulevya na kabla ya kurejea nchini, alikuwa akitumikia kifungo barani Asia.
Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova alisema jana, wamekamata pipi 33 za dawa za kulevya aina ya Heroine zenye thamani ya mamilioni ya fedha.
Alisema baada ya polisi kupata taarifa ya tukio hilo, walikwenda nyumbani kwa Rajabu maeneo ya Tabata na kumhoji, ambapo waligundua uwepo wa maiti sebuleni, ikiwa imelazwa chali katika godoro.
Kwa mujibu wa Kova, Rajabu ndiye mmiliki wa chumba kilichokutwa maiti na uchunguzi unaonyesha marehemu alifika juzi kutoka Mtwara.
Alisema imebainika kuwa kabla ya kifo cha mfanyabiashara huyo, alikwenda bafuni kuoga na alirudi katika chumba hicho na ndipo alipokutwa na umauti.
Kamishna huyo alisema mazingira ya kifo hicho ndiyo yaliyosababisha polisi kupata taarifa na walipofika eneo la tukio, waliuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi.
Alisema mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi na madaktari wawili, ukishuhudiwa na maofisa wa polisi na ndugu za marehemu, na kwamba alikutwa na pipi 33 za dawa za kulevya.
Kova alisema uchunguzi unaendelea ili kubaini mtandao wa usafirishaji wa dawa hizo, ambao umehusisha marehemu na watakaokamatwa watachukuliwa hatua za kisheria.
Alisema marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria ambayo haikuonyesha anasafiri kwenda nchi gani.
Kova alisema marehemu alikutwa na vitu mbalimbali, ikiwemo fedha taslimu za Kenya sh. 700, dola 100 za Marekani (sh. 160,000), pamoja na fedha za Shelisheli 100.

DC Tarime matatani


NA SULEIMAN JONGO, TARIME
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeingilia kati mgogoro wa muda mrefu kati ya mgodi wa dhahabu wa North Mara, ulioko Nyamongo wilayani Tarime mkoa wa Mara na kuahidi kuupatia ufumbuzi.
Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele, ametajwa kuwa kinara katika kukuza mgogoro, na kwamba ana maslahi binafsi ndani yake.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, juzi alilazimika kuahirisha shughuli zote alizopangiwa akiwa wilayani humo, ikiwemo baadhi ya mikutano ya hadhara ili kupata muda wa kukutana na pande zote zinazohusika na mgogoro huo.
Kinana alilazimika kuchukua hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka pande mbalimbali, ikiwemo taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo dhidi ya mgodi huo.
Akiwahutubia wananchi wa Nyamongo, Kinana alisema CCM ndicho Chama chenye serikali, hivyo haiwezi kuungana na walalamikaji badala yake imedhamiria kumaliza tatizo hilo.
Alisema tatizo hilo lazima limalizwe mara moja ili wananchi wa Nyamongo na wote wanaouzunguka mgodi huo waishi kwa amani na kunufaika na madini yaliyopo.
Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, ametakiwa kumshauri Rais Jakaya Kikwete, ili aweze kumuhamisha Henjewele ambaye anadaiwa kutafuna fedha za malipo ya ada ya wanafunzi zinazotolewa na mgodi wa Barrick North Mara.
Taarifa ya CCM ya wilaya hiyo iliyosomwa mbele ya Kinana na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kemambo, Rashid Gamaina, ilisema Henjewele amekuwa akichochea mgogoro huo kwa kutoa kauli za kejeli na kuwadhalilisha wananchi wa Nyamongo.
Alisema mkuu huyo wa wilaya alifanya ziara Desemba 31, 2010 katika vijiji vya Nyangoto na Kewanja na kutoa maneno ya kejeli ambayo yaliwadhalilisha watu wa vijiji hivyo.
Kwa mujibu wa Gamaina, mgodi huo uliingia makubaliano na wananchi wanaouzunguka ya kuwalipia ada watoto wao walio kwenye shule na vyuo mbalimbali, jambo ambalo hivi sasa halifanyiki.
“Kitu cha kusikitisha ni kuwa, licha malipo hayo kutositishwa, lakini wanafunzi walengwa hawanufaiki nayo kwa kuwa Henjewele amehamishia malipo hayo ofisini kwake.
“Yeye ndiye anayepanga na kuamua nani, huku akipata fursa ya kufanya mambo ya hovyo, ikiwemo kuwalipia wanafunzi kutoka nchini Kenya badala ya wana Nyamongo kama ilivyokusudiwa,” alisema.
Gamaina alimuomba Kinana kumshauri Rais Kikwete, kumhamisha Henjewele wilayani Tarime kwa kuwa uwepo wake utaendelea kuzorotesha uhusiano wa Chama na wananchi.
Hata hivyo, Henjewele alikanusha madai hayo na kusema fedha zinazotolewa na mgodi kwa ajili ya ada zinawafikia walengwa wote.
Akizungumza katika mkutano huo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele aliamuru kusitishwa mara moja kwa mpango huo wa ulipaji ada hadi pale utakapopitiwa na kupangiwa utaratibu mzuri.
Masele alisema baadhi ya viongozi wa ngazi za chini wamekuwa wakiwadanganya wale wa ngazi za juu kwa kuwapa taarifa zisizo sahihi, jambo linalozidisha hasira za wananchi.
Alisema binafsi aliwahi kudanganywa alipotaka kutembelea kijiji cha Nyamongo muda mfupi baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo, huku waliomdanganya wakisema wananchi wa kijiji hicho ni wakorofi na endapo atakwenda amani inaweza kuvunjika.
Kinana aliahidi kumuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani, kufika eneo hilo na kuzungumza na wananchi, ikiwa ni moja ya hatua za kutatua kero zinzowakabili, ikiwemo ya kuwindwa kwa askari wanaolinda mgodi wa Nyamongo.

UFISADI MANISPAA BUKOBA



Utouh atuma salamu  na mwandishi wetu

MKAGUZI Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, amesema mchakato wa kuanza kukagua hesabu za Manispaa ya Bukoba umekamilika na wiki ijayo kazi itaanza rasmi.
Pia, amewatumia salamu baadhi ya watu waliodai hatakwenda kufanya kazi hiyo kama alivyoagizwa na Rais Jakaya Kikwete, kuwa kwa sasa yuko njiani kwenda Bukoba.
Utouh ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza katika semina ya wahariri, ambapo amesema tayari ameunda timu maalumu itakayofanya kazi hiyo kwa kufuata hadidu za rejea walizopewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, ambayo ndio msimamizi wa halmashauri zote nchini.
‘’Tumeshaunda timu maalumu baada ya kupata hadidu za rejea, sasa waambieni watu wa Bukoba waliodhani kuwa hatuendi kuwa tuko barabarani tunawafuata,’’ alisema Utouh.
Ukaguzi huo maalumu unafanyika kutokana na kuibuka kwa madai ya ufisadi unaodaiwa kufanywa na Meya wa Manispaa ya Bukoba, Dk. Anatory Amani, hivyo kuzusha mgogoro mkubwa baina yake na Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki.
Mgogoro huo ulisababisha kuvuliwa uanachama kwa madiwani wanane, ambapo baadaye ulijadiliwa kwenye Kamati Kuu ya CCM na kisha NEC na kutolewa uamuzi kuwa madiwani hao ni halali, huku baadhi ya viongozi wakipewa onyo kali.
Utouh alieleza kushangazwa na baadhi ya vyombo vya habari (si Uhuru) vilivyodai kuwa, ofisi yake imegoma kufanya kazi, akisema hawezi kufanya hivyo kwa kuwa ni wajibu wake kukagua hesabu za serikali.
‘’Huu ni wajibu wangu, hivyo kamwe siwezi kugomea maagizo ya kiongozi wangu, ninakwenda kuifanya kazi hiyo wiki ijayo na kila kitu kiko sawa,’’ alisema.
Awali, Utouh aliviasa vyombo vya habari kutoa taarifa sahihi kuhusu sera na utekelezaji wa mipango mbalimbali katika ofisi yake, kwani baadhi ya taarifa zimekuwa zikipotoshwa.
Alisema baadhi ama kwa kutambua au kwa makusudi, vimekuwa vikitoa taarifa potofu kuhusu ofisi yake, jambo ambalo ni kuwapotosha wananchi na kuwanyima haki ya msingi.
‘’Wapo ambao huangalia utamu wa kuongeza mauzo, lakini hawatazami athari inayoweza kutokea hapo baadaye. Tumeanza mikakati mbalimbali ya kutoa elimu mbadala kwa wadau wetu ili taarifa zinazotolewa ziwe za uhakika na zenye tija kwa taifa,’’ alisema Utouh.



Wednesday 18 September 2013

Kikwete awazodoa wanasiasa waongo

Na Mwandishi Wetu, San Francisco, California
RAIS Jakaya Kikwete ameshangazwa na kiwango cha uongo cha baadhi ya wanasiasa, hasa madai kuwa aliteua wajumbe wa Tume ya Katiba bila kuongozwa na mapendekezo ya wadau mbalimbali waliopendekeza majina hayo.
Aidha, amesema kuwa bado anaendelea kuamini kuwa mchakato wa Katiba Mpya utafikia mwisho wake mwakani, hivyo kuiwezesha Tanzania kufanya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 chini ya Katiba Mpya.
Vilevile, Rais Kikwete amesema kuwa hana tatizo na watu wanaopinga sera za serikali au hata kumpinga yeye binafsi, bali tatizo lake ni wanasiasa na wanaharakati wanaochochea ghasia, fujo na uvunjifu wa amani.
Rais Kikwete aliyasema hayo juzi, mjini San Rafael, California, alipokutana na kuzungumza na jumuia ya Watanzania waishio jimbo hilo nchini Marekani, wakati alipoanza ziara yake ya siku mbili, ikiwa ni sehemu ya ziara ya Marekani.
Katika hotuba yake, ambapo alizungumzia mambo mbalimbali, Rais Kikwete aligusia mjadala wa karibuni Bungeni kuhusu mchakato wa Katiba Mpya na kusema kuwa, alishangazwa na madai kuwa yeye kama Rais hakuongozwa na mapendekezo ya wadau wakati anateua Tume ya Katiba.
“Watu wote niliowateua walipendekezwa na wadau mbali mbali, zikiwemo taasisi za dini. Yule Mama Maria Kashonda alipendekezwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Mama Mwantumu Malale alipendekeza Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
“Kila kundi ambalo lilipendekeza watu limepata mjumbe katika tume hiyo, wakiwemo walemavu ambao naambiwa nimewasahau,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Hivi nyie wanasiasa wenzangu mkikosa hoja mnaongopa hata kwa vitu ambavyo viko wazi kabisa. Tulikubaliana kuwa Rais angefanya uteuzi wa wajumbe wa tume baada ya kupokea mapendekezo ya wadau mbali na katika mchakato ulioendeshwa kwa uwazi kabisa. Hivyo, ndiyo ilivyofanyika. Sasa uongo wa nini? Kama hakuna hoja ni kwamba hakuna tu na wala uongo hautasaidia.”
Kuhusu kama Tanzania itaweza kupata Katiba Mpya kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Rais Kikwete amesema: “Ningependa sana, na kwa kweli ni matarajio yangu makubwa kuwa, tuweze kumaliza mchakato wetu mwaka 2014 na tuweze kuwa na Katiba Mpya ili iongoze Uchaguzi Mkuu wetu wa mwaka 2015.
‘’Mchakato wetu unakwenda vizuri na wala siyo lazima tuhangaike na Katiba kwa miaka mingi. Muhimu ni ushirikishwaji wa kila mmoja wetu.”
Akizungumzia tabia za wanasiasa wa Tanzania kwa jumla, hasa wale wanaochochea chuki na ghasia, Rais Kikwete aliwaambia Watanzania hao:
“Sina tatizo na wanasiasa au wanaharakati kupinga sera za serikali yangu. Hili ni suala la nguvu ya hoja na tunao uwezo mkubwa wa kutetea sera zetu. Na wala sina tatizo na watu kunipinga mimi binafsi. Kinachonipa taabu ni pale wanasiasa na wanaharakati wanapochochea ghasia na kuleta fujo. Kama mtu anataka kuongoza Tanzania si asubiri hadi atakapochaguliwa?”
Rais Kikwete aliongeza: “Hivi unapochochea ghasia, fujo na chuki na kweli mambo hayo yakatokea na nchi ikateketea, utaongoza nchi ya namna gani? Utaongoza magofu na majivu yatakayobakia baada ya nchi kuteketea?”
Kuhusu mjadala wa karibuni kuhusu kama Rais awe na madaraka ya kuteua wajumbe 166 wa nyongeza ili kuingia katika Bunge la Katiba kujadili Rasimu ya Katiba Mpya, Rais Kikwete alisema kuwa yeye hana taabu kama itabidi ateua basi atateua, lakini kama siyo lazima yeye hana taabu.
“Mimi sina taabu, wakisema niteue, basi nitateua. Wakisema nisiteua vilevile sina taabu, isitoshe hiyo itakuwa inanipungumzia mzigo na kazi. Ile kazi yenyewe ya kuteua wajumbe wa Tume ya Katiba haikuwa rahisi.”
Rais Kikwete alitumia siku ya pili ya ziara yake katika Jimbo la California kwa kutembelea Jiji la Vallejo, ambako alikutana na Meya wa Mji huo, Osby Davis, pamoja na madiwani wa jiji hilo na wafanyakazi wake.
Ziara hiyo ya Rais Kikwete katika Jiji la Vallejo, nje ya Jiji la San Francisco, imekuja wakati wa Kumbukumbu ya Miaka 20 tangu jiji hilo lianzishe uhusiano wa kidada na mji wa Bagamoyo ulioko mkoa wa Pwani ulioanzishwa mwaka 1993.
Rais Kikwete alitumia muda mwingi wakati wa mkutano na baadaye wakati wa chakula cha mchana na viongozi wa jiji hilo kujenga hoja ya kuvutia wawekezaji wa Jiji la Vallejo kuwekeza katika uchumi wa Tanzania.
Pia, Rais Kikwete aliwaelezea viongozi wa jiji hilo kuhusu historia ya mji wa Bagamoyo na asili ya jina la mji huo lilitokana na enzi ya watumwa ambako mji uliitwa Bwaga Moyo (Tuliza Moyo Wako).
0000
...awatosa wauza unga
“Ukikamatwa na dawa za kulevya hatukutetei, hatuwezi kuendelea kuwa na sifa ya kufanya biashara za ovyo ovyo kiasi hicho.
Na Mwandishi Wetu, San Francisco, California
RAIS Jakaya Kikwete amesema serikali yake haitawatetea Watanzania wanaokamatwa wamebeba dawa za kulevya nje ya nchi kwa sababu biashara hiyo ni haramu.
Aidha, amesema kuwa serikali yake haina uhakika kama suala la uraia pacha (dual citizenship) litaweza kuwemo katika Katiba Mpya kwa sababu suala hilo halikuwamo katika Rasimu ya Katiba hata kama limependekezwa tena na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Rais Kikwete amesema ni wajibu wa Watanzania wanaoishi ughaibuni kuwa raia wema na kufuata na kuheshimu sheria katika nchi wanazoishi kwa sababu wakivunja sheria za nchi hizo serikali yake haitawatetea.
Alitoa ufafanuzi huo juzi alipokutana na kuzungumza na Watanzania wanaoishi katika Jimbo la California, Marekani, kwenye siku ya kwanza ya ziara yake ya siku mbili katika jimbo hilo.
Akizungumza na Watanzania hao katika Hoteli Embassy iliyoko San Rafael, Rais Kikwete, alisema ni kweli Watanzania wamejiingiza kwa kiasi kikubwa katika ya biashara za ovyo ovyo, ikiwemo dawa za kulevya, lakini serikali yake haitawatetea Watanzania wanaokamatwa.
“Ukikamatwa na dawa za kulevya hatukutetei kwa sababu hata sheria za nchi zetu zinazuia biashara hiyo. Sisi hatuwezi kuendelea kuwa na sifa ya kufanya biashara za ovyo ovyo kiasi hicho.
“Serikali itawatetea Watanzania wanaoishi nchi za nje ikiwa wataonewa. Lakini ukifanya biashara ya dawa za kulevya au kubaka watu hatukutetei kamwe,” alisisitiza Rais Kikwete.
Kuhusu suala la uraia pacha kuwekwa katika Katibu Mpya, Rais Kikwete alisema kuwa katika maoni ya awali suala hilo halikusikika kiasi cha Wajumbe wa Tume ya Katiba kuliweka katika Rasimu ya Katiba.
“Lakini sisi katika CCM tumelizungumza na kuliweka katika mapendekezo yetu mapya tulipokaa kama Baraza la Katiba. Tunataka lizungumzwe. Hatuna hakika kama litawekwa katika rasimu ijayo, lakini tutaendelea kulisemea.
“Kubwa ni kwamba hili ni jambo ambalo halitapata sauti za kutosha kulisemea. Lakini faida zake zinaeleweka hata kama inaelekea kuwa hakuna watu wengi wanaokereketwa na jambo hili kiasi cha kulisema kiasi cha kutosha katika mjadala wa Katiba.”
Hata hivyo, Rais Kikwete aliwashauri Watanzania wanaoishi nchi za nje kuishi kwa amani, kuheshimu sheria na kutojiingiza katika mambo yanayoweza kuwaingiza katika matatizo.
“Lazima muwe raia wema. Mliamua wenyewe kuja kuishi katika nchi hizi. Nchi hizi zina sheria zake. Kama mtaamua kuwa raia wabaya wanaovunja sheria mtaingia katika matatizo – kama wasemavyo Waingereza ‘you will face the music and sometimes that music may not be enjoyable.”
Kuhusu ombi la Watanzania waishio nje  kuruhusiwa kupiga kura, Rais Kikwete alisema serikali yake haina tatizo wala pingamizi na suala hilo ili mradi tu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iwe na uwezo wa kulifanikisha jambo hilo. “Kama wanaweza hakuna kipingamizi. Hatuna matatizo na jambo hili.”



Wakulima wa pamba waishukia CHADEMA

na mwandishi wetu, Simiyu
HATUA ya CHADEMA kumshambulia Balozi wa China nchini, Dk. Lu Youqing kwa kupanda jukwaani kuelezea mambo mazuri ambayo serikali ya nchi hiyo imepanga kuwafanyia wakazi wa Shinyanga, hususan wakulima wa pamba, imewakera wananchi na kuwaonya viongozi wa chama hicho kuacha kuweweseka.
Wamesema siasa za chuki na hila zinazofanywa na viongozi wa CHADEMA dhidi ya Balozi Dk. Lu zimewakera, na kwamba hatua za kuanzisha viwanda na kuokoa zao la pamba zinazofanywa na serikali ya China zinapaswa kuungwa mkono na yeyote, na mwenye kupinga hana mapenzi mema na wakulima nchini.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wakulima hao walimweleza Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kuwa, wamechukizwa na hila na ghilba zinazoendeshwa na CHADEMA kwa kushirikiana na vyama vingine kupinga hatua za China katika kuwakomboa Watanzania kwa kuwaletea maendeleo ya kweli.
‘’Kwa muda mrefu wakulima wa pamba tunakabiliwa na changamoto nyingi, sasa wenzetu ambao ni marafiki wa kweli wameamua kuchukua hatua za kutusaidia, lakini wanasiasa wachache kwa maslahi yao wameamua kupotosha ukweli.
“Kumshambulia balozi kwa kupanda jukwaani kueleza mambo ya maendeleo wanayotufanyia si uungwana na inaonyesha wazi namna ambavyo viongozi wa CHADEMA walibvyo wanafiki na hawana mapenzi ya dhati na Watanzania, hususan wa Kanda ya Ziwa ambao wanategemea zao hili kujiletea maendeleo,’’ alisema Shija Mabula kwa niaba ya wananchi wenzake.
Alisema viongozi wa CHADEMA, akiwemo Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa, wamekuwa vinara wa kuendesha siasa za chuki zenye lengo la kuwagombanisha wananchi na serikali badala ya kuwa mstari wa mbele kuhamasisha maendeleo kupitia siasa safi na zenye tija.
“CHADEMA wamechanganyikiwa, kwa sababu siku zote wamekuwa wakitegemea kuendesha chama chao kwa mgongo wa umasikini wa Watanzania, sasa kasi ya kutengeneza ajira kupitia ujenzi wa viwanda, na mchakato wa kuwezesha kuongeza bei ya mazao ili kuwakwamua wakulima kutoka katika umasikini umewachanganya,” alisema Mabula.
Kwa upande wake, Nape aliwaasa wananchi hao kuwapuuza viongozi wa CHADEMA, kwani kazi nzuri inayofanywa na serikali ya CCM katika kuwaletea Watanzania maendeleo imekuwa ikiwakera na ndio sababu wamekuwa wakitafuta njia za kuanzisha vurugu ili kuikwamisha.
Hata hivyo, alisema serikali ya CCM kwa kushirikiana na washirika wake itaendelea kuhakikisha inatekeleza kila ilichoahidi kuwafanyia wananchi, na kwamba hila na ghilba zinazofanywa na viongozi wa CHADEMA kamwe haziwezi kufanikiwa.
Alisema kikubwa kilichowakera CHADEMA ni kuona jitihada za serikali ya CCM na China zinakaribia kuzaa matunda kupitia ujenzi wa viwanda vya pamba, ambavyo pamoja na mambo mengine vitatoa ajira kwa zaidi ya watu 25,000.
Nape, huku akiwa amezungukwa na maelfu ya wananchi katika viwanja vya CCM Sabasaba mkoani Simiyu, alisema mtaji mkubwa wa CHADEMA kisiasa ni tatizo la ajira kwa vijana na kwamba, jitihada za kumaliza tatizo hilo zinazochukuliwa ni pigo kwao, kwani watakosa watu wa kuwaunga mkono kwenye maandamano.
“Tayari tumeshaingia makubaliano na Serikali ya China ya kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani ya mazao kama vile pamba, ufuta, alizeti na mazao ya mifugo, ikiwemo ngozi za ng’ombe, hivyo chuki na hasira ya CHADEMA dhidi ya Balozi wa China inasababishwa na mafanikio hayo ya kutatua matatizo ya wananchi,” alisema Nape.
Pia, Nape alionyesha kushangazwa na viongozi wa CHADEMA kulalamika kuhusu kilichofanywa na Balozi Dk. Lu wakati si yeye pekee aliyewahi kuhudhuria shughuli za CCM, ikiwemo Mkutano Mkuu, vikao vya Bunge pamoja na kumtembea Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ofisini kwake, lakini hawakuwahi kupiga kelele kama ilivyo sasa.
‘’Hili ni pigo kwa CHADEMA, kwani watakosa watu wa kuwaunga mkono katika kelele zao na maandamano, mabalozi wengi wamekuwa wakihudhuria sherehe za CCM, ikiwemo kumtembelea Kinana ofisini, zaidi ya nusu ya mabalozi wameshafanya hivyo, mbona hawakupiga kelele na kushitakiwa Umoja wa Mataifa.
“Hili la Balozi Dk. Lu kupanda jukwaani na kueleza kitu gani serikali ya China itakachowafanyia wananchi imekuwa nongwa,’’ alihoji Nape.
Akifafanua, alisema balozi huyo alishawahi kutembelea na kufanya ukaguzi wa ujenzi wa makao makuu ya Chama na Chuo Kikuu cha Chama, Ihemi mkoani Iringa, lakini hakukuwa na malalamiko kutoka CHADEMA.
“Kinachowaumiza CHADEMA ni kuona mtaji wao wa kisiasa wa kuwatumia watu kupiga kelele na kufanya maandamano yasiyo na tija sasa umekwisha,” alisema.
Ends.






KESI YA MRAMBA NA YONA

NA FURAHA OMARY
MCHAKATO wa kumpata mkaguzi wa madini ya dhahabu ulifanywa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwa maagizo ya aliyekuwa Gavana wa Benki hiyo, Dk. Daud Ballali (sasa marehemu), imedaiwa.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha wa BoT, Kessi-Sia Mbatia (61), alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alipokuwa akitoa ushahidi katika kesi inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake.
Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni waliokuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja.
Mramba na wenzake wanakabiliwa na mashitaka ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia serikali hasara ya sh. bilioni 11.7 kutokana na kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni iliyoshinda zabuni ya ukaguzi wa madini ya dhahabu ya Alex Stewart.
Kessi, ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya watu watano walioshughulikia mchakato wa kumpata mkaguzi huyo, alidai hayo mbele ya jopo la mahakimu likiongozwa na Jaji John Utamwa, akiwa shahidi wa Mramba. Mahakimu wengine katika jopo hilo ni Jaji Sam Rumanyika na Saul Kinemela.
Akiongozwa na Wakili Hurbert Nyange, anayemtetea Mramba kutoa ushahidi, Kessi alidai kwa sasa ni mkulima na mshauri mtaalamu, baada ya kustaafu kazi mwaka 2009. Alidai aliajiriwa na BoT tangu mwaka 1975 hadi 2009 kwa  ajira ya kudumu na Desemba 2009 hadi Septemba 2010, alikuwa akifanya kazi kwa mkataba.
Shahidi huyo, alidai kuanzia mwaka 2000 hadi 2005, alikuwa Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha wa BoT, na kwamba alihusika katika mchakato wa kumpata mkaguzi wa dhahabu kwa maagizo ya Dk. Ballali.
Alidai maagizo hayo alipewa mwishoni mwa mwaka 2002 ya kusimamia kamati aliyoiteua ya watu watano, akiwemo yeye kushughulikia mchakato huo, na kwamba walikuwa wakiwasilisha ripoti kwa gavana.
Kessi alidai wajumbe wa kamati hiyo walikuwa kutoka Wizara ya Nishati na Madini (mmoja), maofisa wa BoT (wawili) na mshauri wa gavana. Alidai kamati hiyo ya awali, baadaye iliongezewa wawakilishi kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
Shahidi huyo alidai kamati ya awali ilifanya kazi ya kuingia katika mtandao kutafuta kampuni za kufanya kazi hiyo, ambapo walipata orodha ya kampuni 21 na baadaye walizichambua na kubaki tano na kuzipeleka taarifa ambapo mbili ziliwasilisha taarifa zao.
ìBaada ya kuchambua taarifa hizo, tulihitimisha kwamba kampuni ya Alex Stewart inastahili kupata kazi hiyo kwa bei ya asilimia 1.9. Tulipeleka mapendekezo yetu kwa gavana ambaye alitutuma kazi, baadaye aliitwa mwakilishi wa kampuni hiyo kufanya makubaliano na hatimaye kupewa mkataba,î alidai.
Sehemu ya ushahidi wa Kessi kwa mtindo wa maswali na majibu akiongozwa na Wakili Nyange ni ifuatavyo:
Nyange; Wakati mnafanya mchakato wa kumtafuta mkandarasi huyo, mlikuwa mnaripoti kwa nani?
Shahidi: Kazi tukimaliza ripoti tunapeleka kwa gavana.
Nyange: Wewe ulikuwa mwajiri wa gavana na gavana alikuwa mwajiri wake nani?
Shahidi: Rais
Nyange: Unamfahamu mshitakiwa aliyesimama (Mramba) na ieleze mahakama unamfahamu vipi?
Shahidi: Ndio, namfahamu kama mwanasiasa na aliwahi kuwa Waziri wa Fedha.
Nyange: Ni kwa kiasi gani mshitakiwa (Mramba) alihusika katika mchakato huo?
Shahidi: Kwa ngazi yangu nisingeweza kujua kwa sababu nilikuwa naripoti kwa gavana na kuishia hapo.
Nyange: Nani alimwalika mwakilishi wa Alex Stewart kuja kufanya makubaliano ya mkataba?
Shahidi: BoT na yalifanywa baina ya kamati na mkandarasi.
Baada ya kuonyeshwa kielelezo ambacho ni mkataba baina ya kampuni hiyo na BoT, shahidi huyo alidai kampuni hiyo ilikuwa iko tayari kuchukua bei ya asilimia 1.9 baada ya kutoa kodi zote.
Pia, alidai kulingana na mkataba mkandarasi huyo ilikuwa afanye kazi kwa miaka miwili, ambapo baadaye aliongezewa miaka miwili mingine kutokana na barua aliyoandikiwa na Gavana Dk. Ballali ya kumteua kuja kutia saini mkataba.
Shahidi huyo alidai mkandarasi huyo alipokuja alikuwa tayari ameshateuliwa, hivyo kamati yao haikuwa na kazi kubwa na hata walipotaka kukaa naye mezani kujadiliana hakuwa tayari kwa madai barua iliyomteua ilimpa haki kama za awali.
Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.




Lukuvi aipa maagizo NFRA




SERIKALI imeiagiza Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), kuzingatia ubora na usafi katika ununuzi wa mahindi.
Imesema mahindi hayo yananunuliwa kwa ajili ya chakula kwa Watanzania, hivyo ni lazima yawe na ubora unaokubalika.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, wakati akizungumza na watendaji wa wakala huo katika ziara ya kukagua vituo vya mahindi.
Katika ziara hiyo Lukuvi alikagua vituo vya Mtenga, Namanyere na Kasu vilivyopo wilayani Nkasi, ambapo alipokea taarifa ya ununuzi wa mahindi katika vituo hivyo.
ìItakuwa sio vyema kununua mahindi ambayo yako chini ya kiwango na yaliyo na uchafu mwingi kwa kuwa yananunuliwa kwa matumizi ya chakula ni si vinginevyo. Ni lazima yawe masafi na yenge viwango bora kwa walaji.
ìMwaka huu serikali imetoa bei nzuri ya sh. 500 kwa kilo kwa kuzingatia uhitaji, kutokana na bei hiyo NFRA inatakiwa kununua mahindi yaliyo safi ili kuweza kupanga viwango tofauti ambavyo vitawasaidia katika uuzaji,íí alisema.
Alisema mwaka huu, serikali ndio mnunuzi mkubwa wa mahindi nchini na NFRA ndiyo inayoongoza katika ununuzi huo, hivyo kuagiza kuanza usafirishaji wa mahindi kwenda mkoani Shinyanga mapema kabla kipindi cha mvua kuanza.


Pinda ahidi serikali kuzidi kushirikisha ngazi za chini


Na Jesca Kileo
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema serikali itaendelea kushirikiana na wabia wa maendeleo ili kuimarisha utawala bora na hatimaye kusaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi katika ngazi za chini.
Pia, ameagiza watendaji wa ngazi za chini kutoa taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi badala ya kuzificha, kwani hatua hiyo itasaidia kuongeza uwazi na kujenga imani kwa wananchi wanaowaongoza.
Alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua maadhimisho ya Siku ya Soko la SULGO yaliyoandaliwa na TAMISEMI kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Maendeleo ya Ujerumani (GZI).
Alisema maonyesho hayo yamelenga kujenga uwezo kwenye serikali za mitaa ili waweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi kwa kuwapatia mafunzo yatakayowawezesha kuwa na vyanzo vya fedha, kuwekewa mifumo ya kupata fedha hizo, kuwezeshwa kusimamia matumizi ya fedha zao na kujengewa ushirikishwaji wa wananchi kuanzia ngazi ya chini hadi taifa.
ìSerikali za Mitaa ndiyo nyenzo kuu ya serikali katika utekelezaji wa shughuli za serikali, na fedha nyingi zinapelekwa huko ambako miradi ya maendeleo iko. Utaona kuna fedha ni jambo moja lakini kuweza kusimamia matumizi ya zile fedha ni jambo lingine kwa hiyo wametoa mafunzo kwa watendaji wa vijiji na kata juu ya suala hili,î alisema.
Akizungumza na waadishi wa habari baada ya kukagua maonyesho hayo, Waziri Mkuu Pinda, alisema amefurahi kuona katika ngazi ya chini kabisa wananchi wamejengewa uwezo wa kutambua jinsi sheria ndogo zinavyotungwa.
Aliishukuru Serikali ya Ujerumani kupitia GIZ ambayo imetoa Euro milioni 9.8 kwa ajili ya kusaidia mradi huo unaotekelezwa kwa majaribio kwenye wilaya za mikoa ya Tanga na Mtwara. Wilaya hizo ni Mtwara, Nanyumbu, Tandahimba na Masasi kwa mkoa wa Mtwara wakati mkoani Tanga unatekelezwa katika wilaya za Handeni, Muheza, Jiji la Tanga na wilaya ya Tanga.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu, kufungua maonyesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Hawa Ghasia, alisema soko la SULGO ni dhana ya ushirikishwaji wa wananchi katika kutoa maamuzi kuanzia ngazi ya chini, ngazi ya wilaya na hatimaye ngazi ya taifa au serikali kuu.
Alisema dhana hiyo, imekuwa ikiendeshwa chini ya Mpango wa Serikali wa Maboresho ya Serikali za Mitaa (LGRP). Alisema mradi huo wa Soko la SULGO ulianza Januari 2008 na unatarajiwa kukamilika Septemba mwakani.
Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano kutoka Ubalozi wa Ujerumani, Claudia Imwolde-Kraemer, alisema mradi huo umelenga kuimarisha utendaji wa serikali za mitaa kwa kufuatilia ukusanyaji wa mapato na kuweka mifumo ya uwajibikaji kwenye masuala ya fedha.

Pinda ahidi serikali kuzidi kushirikisha ngazi za chini


Na Jesca Kileo
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema serikali itaendelea kushirikiana na wabia wa maendeleo ili kuimarisha utawala bora na hatimaye kusaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi katika ngazi za chini.
Pia, ameagiza watendaji wa ngazi za chini kutoa taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi badala ya kuzificha, kwani hatua hiyo itasaidia kuongeza uwazi na kujenga imani kwa wananchi wanaowaongoza.
Alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua maadhimisho ya Siku ya Soko la SULGO yaliyoandaliwa na TAMISEMI kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Maendeleo ya Ujerumani (GZI).
Alisema maonyesho hayo yamelenga kujenga uwezo kwenye serikali za mitaa ili waweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi kwa kuwapatia mafunzo yatakayowawezesha kuwa na vyanzo vya fedha, kuwekewa mifumo ya kupata fedha hizo, kuwezeshwa kusimamia matumizi ya fedha zao na kujengewa ushirikishwaji wa wananchi kuanzia ngazi ya chini hadi taifa.
ìSerikali za Mitaa ndiyo nyenzo kuu ya serikali katika utekelezaji wa shughuli za serikali, na fedha nyingi zinapelekwa huko ambako miradi ya maendeleo iko. Utaona kuna fedha ni jambo moja lakini kuweza kusimamia matumizi ya zile fedha ni jambo lingine kwa hiyo wametoa mafunzo kwa watendaji wa vijiji na kata juu ya suala hili,î alisema.
Akizungumza na waadishi wa habari baada ya kukagua maonyesho hayo, Waziri Mkuu Pinda, alisema amefurahi kuona katika ngazi ya chini kabisa wananchi wamejengewa uwezo wa kutambua jinsi sheria ndogo zinavyotungwa.
Aliishukuru Serikali ya Ujerumani kupitia GIZ ambayo imetoa Euro milioni 9.8 kwa ajili ya kusaidia mradi huo unaotekelezwa kwa majaribio kwenye wilaya za mikoa ya Tanga na Mtwara. Wilaya hizo ni Mtwara, Nanyumbu, Tandahimba na Masasi kwa mkoa wa Mtwara wakati mkoani Tanga unatekelezwa katika wilaya za Handeni, Muheza, Jiji la Tanga na wilaya ya Tanga.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu, kufungua maonyesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Hawa Ghasia, alisema soko la SULGO ni dhana ya ushirikishwaji wa wananchi katika kutoa maamuzi kuanzia ngazi ya chini, ngazi ya wilaya na hatimaye ngazi ya taifa au serikali kuu.
Alisema dhana hiyo, imekuwa ikiendeshwa chini ya Mpango wa Serikali wa Maboresho ya Serikali za Mitaa (LGRP). Alisema mradi huo wa Soko la SULGO ulianza Januari 2008 na unatarajiwa kukamilika Septemba mwakani.
Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano kutoka Ubalozi wa Ujerumani, Claudia Imwolde-Kraemer, alisema mradi huo umelenga kuimarisha utendaji wa serikali za mitaa kwa kufuatilia ukusanyaji wa mapato na kuweka mifumo ya uwajibikaji kwenye masuala ya fedha.

CHADEMA yadaiwa kipoteza mwelekeo


Na Mwandishi Wetu, Morogoro
NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi (Bara) Glorious Luoga, amekiponda CHADEMA kwa madai kuwa kimepoteza mwelekeo kisiasa kutokana na kuendesha sera za chuki na matusi dhidi ya viongozi wa CCM.
Alisema sera za namna hiyo kamwe hazikubaliki na hazipaswi kupewa nafasi katika jamii kwa kuwa zinaashiria uvunjifu wa amani na utulivu uliopo nchini.
Luoga alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliyofanyika Gairo mkoani Morogoro.
Alisema CHADEMA kimeshindwa kufanya shughuli zake kama chama cha kisiasa kwa kunadi sera zake na badala yake viongozi wake wamekuwa wakipanda katika majukwaa na kuanza kuwashambulia kwa matusi viongozi wa CCM.
Hata hivyo, Luoga aliwafananisha viongozi hao wa CHADEMA na watoto waliokuwa wakiishi maisha ya tabu na njaa kali kwa kipindi kirefu, lakini baada ya kupewa chakula na kushiba wakasahau shida iliyowapata na kuanza kutukana wazazi wao waliowapa chakula.
ìHakuna asiyejua kama CHADEMA sasa wamelewa shibe baada ya kuonewa huruma na kupata viti vichache vya madiwani na wabunge.
ìKabla ya kupata viti hivyo kimekuwa kikiendesha sera za kiustaraabu, lakini sasa kimejijengea utamaduni wa kulazimisha kutumia lugha ya matusi dhidi wa CCM waliowafundisha siasa na mpaka kufikia hapo kilipo,î alisema Luoga.
Alisema CCM haitishiki na siasa hizo uchwara na badala yake itazidi kujikita kuimarisha Chama hicho na kutekeleza Ilani yake ya uchaguzi kwa kuwaletea maendeleo wananchi wake bila kujali itikadi za kisiasa, rangi, kabila wala dini.
Luoga aliwataka wananchi wa Gairo wasikubali kufanya makosa kwa mara nyingine katika uchaguzi mkuu ujao kwa kuchagua wagombea wa vyama vya upinzani.

CHADEMA yadaiwa kipoteza mwelekeo


Na Mwandishi Wetu, Morogoro
NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi (Bara) Glorious Luoga, amekiponda CHADEMA kwa madai kuwa kimepoteza mwelekeo kisiasa kutokana na kuendesha sera za chuki na matusi dhidi ya viongozi wa CCM.
Alisema sera za namna hiyo kamwe hazikubaliki na hazipaswi kupewa nafasi katika jamii kwa kuwa zinaashiria uvunjifu wa amani na utulivu uliopo nchini.
Luoga alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliyofanyika Gairo mkoani Morogoro.
Alisema CHADEMA kimeshindwa kufanya shughuli zake kama chama cha kisiasa kwa kunadi sera zake na badala yake viongozi wake wamekuwa wakipanda katika majukwaa na kuanza kuwashambulia kwa matusi viongozi wa CCM.
Hata hivyo, Luoga aliwafananisha viongozi hao wa CHADEMA na watoto waliokuwa wakiishi maisha ya tabu na njaa kali kwa kipindi kirefu, lakini baada ya kupewa chakula na kushiba wakasahau shida iliyowapata na kuanza kutukana wazazi wao waliowapa chakula.
ìHakuna asiyejua kama CHADEMA sasa wamelewa shibe baada ya kuonewa huruma na kupata viti vichache vya madiwani na wabunge.
ìKabla ya kupata viti hivyo kimekuwa kikiendesha sera za kiustaraabu, lakini sasa kimejijengea utamaduni wa kulazimisha kutumia lugha ya matusi dhidi wa CCM waliowafundisha siasa na mpaka kufikia hapo kilipo,î alisema Luoga.
Alisema CCM haitishiki na siasa hizo uchwara na badala yake itazidi kujikita kuimarisha Chama hicho na kutekeleza Ilani yake ya uchaguzi kwa kuwaletea maendeleo wananchi wake bila kujali itikadi za kisiasa, rangi, kabila wala dini.
Luoga aliwataka wananchi wa Gairo wasikubali kufanya makosa kwa mara nyingine katika uchaguzi mkuu ujao kwa kuchagua wagombea wa vyama vya upinzani.

CHADEMA yadaiwa kipoteza mwelekeo


Na Mwandishi Wetu, Morogoro
NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi (Bara) Glorious Luoga, amekiponda CHADEMA kwa madai kuwa kimepoteza mwelekeo kisiasa kutokana na kuendesha sera za chuki na matusi dhidi ya viongozi wa CCM.
Alisema sera za namna hiyo kamwe hazikubaliki na hazipaswi kupewa nafasi katika jamii kwa kuwa zinaashiria uvunjifu wa amani na utulivu uliopo nchini.
Luoga alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliyofanyika Gairo mkoani Morogoro.
Alisema CHADEMA kimeshindwa kufanya shughuli zake kama chama cha kisiasa kwa kunadi sera zake na badala yake viongozi wake wamekuwa wakipanda katika majukwaa na kuanza kuwashambulia kwa matusi viongozi wa CCM.
Hata hivyo, Luoga aliwafananisha viongozi hao wa CHADEMA na watoto waliokuwa wakiishi maisha ya tabu na njaa kali kwa kipindi kirefu, lakini baada ya kupewa chakula na kushiba wakasahau shida iliyowapata na kuanza kutukana wazazi wao waliowapa chakula.
ìHakuna asiyejua kama CHADEMA sasa wamelewa shibe baada ya kuonewa huruma na kupata viti vichache vya madiwani na wabunge.
ìKabla ya kupata viti hivyo kimekuwa kikiendesha sera za kiustaraabu, lakini sasa kimejijengea utamaduni wa kulazimisha kutumia lugha ya matusi dhidi wa CCM waliowafundisha siasa na mpaka kufikia hapo kilipo,î alisema Luoga.
Alisema CCM haitishiki na siasa hizo uchwara na badala yake itazidi kujikita kuimarisha Chama hicho na kutekeleza Ilani yake ya uchaguzi kwa kuwaletea maendeleo wananchi wake bila kujali itikadi za kisiasa, rangi, kabila wala dini.
Luoga aliwataka wananchi wa Gairo wasikubali kufanya makosa kwa mara nyingine katika uchaguzi mkuu ujao kwa kuchagua wagombea wa vyama vya upinzani.

Tuesday 17 September 2013

CCM yawaka


NA SULEIMAN JONGO, MEATU
KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, amewataka Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki na Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, kutoka ofisini  na kwenda maeneo yenye migogoro inayotishia damu kumwagika.
Amesema ni kwa njia hiyo ndipo watakapoweza kumaliza migogoro ya ardhi ya wafugaji na wakulima na ile ya wananchi na maeneo ya hifadhi za taifa.
Kinana aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mwasengele kilichoko kwenye jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu akiwa kwenye ziara ya kikazi.
Alisema kuna migogoro mingi maeneo mbalimbali nchini ambayo njia pekee ya kuweza kuitatua ni kwa mawaziri
wanaohusika kwenda kwa wananchi kukaa pamoja na kutafuta suluhu.
Kinana alisema waziri hawezi kutatua mgogoro unaofukuta kati ya wananchi wa Wilaya ya Maswa kuhusu tatizo la maofisa wanyamapori na wafugaji bila kufika eneo husika na kusikiliza kutoka vinywani mwao.
"Kuna migogoro mingi mkoani Morogoro, Wanging'ombe na hapa katika Pori la Akiba la Maswa, lakini ili kuweza kupata ufumbuzi ni lazima kufika kwenye maeneo husika na kusikiliza pande zote, wakiwemo wananchi," alisema.
Katubu Mkuu alisema huu si wakati wa kuendele kutatua migogoro huku mawaziri husika wakiwa ofisini na kuwa sheria zipo kwani hilo
ndilo lililoifikisha migogoro hiyo hapa ilipo.
Aliyasema hayo baada ya kutoa nafasi ya kusikiliza kero za wananchi ambapo mmoja wa waliohudhuria mkutano huo,  Zunzu Ndaturu, alisema kero kubwa inayowakabili wananchi wanaozunguuka pori hilo la hifadhi ni wanyama wakali na maofisa wa hifadhi kuchukua mifugo yao na kuwaomba rushwa mara kwa mara.
Kwa upande wake, Mbunge wa Kisesa, Luhanga Mpina, alisema licha ya serikali kutekeleza miradi mingi ya maendeleo ikiwemo kuboresha barabara na ujenzi wa Daraja la Mto Mongo Bhakima uliokuwa kero kwa wakazi wa eneo hilo, bado inaendelea kutekeleza miradi mingine.

Utata wa kisheria watawala kesi ya 'unga' Dar


NA MWANDISHI WETU
MALUMBANO ya kisheria yameibuka kwa mara nyingine katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili raia wa Kenya, Mwanaidi Mfundo au Mama Leila na wenzake wanane.
Katika malumbano hayo jana baina ya mawakili wa upande wa Jamhuri na wa utetezi, yalihusu uhalali wa notisi iliyowasilishwa mahakamani hapo juzi ya kuitwa mashahidi wawili muhimu wa upande wa Jamhuri akiwemo anayedaiwa kufunga dawa hizo.
Washitakiwa wengine ni  Anthony Karanja na Ben Macharia (Wakenya) na Watanzania Sara Munuo, Almas Said, Yahya Ibrahim, Aisha Kungwi, Rajabu Mzome na John William. Washitakiwa hao wanadaiwa kuingiza nchini dawa za kulevya aina ya cocaine zenye thamani ya sh. milioni 225.
Kabla ya kuanza kwa malumbano hayo jana, Jaji Grace Mwakipesile, alitoa uamuzi juu ya maombi ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Prosper Mwangamila, aliyoyawasilisha juzi wakati kesi hiyo ilipotajwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa.
Juzi, Mwangamila aliiomba mahakama kuahirisha shauri hilo hadi jana ili aweze kuwasilisha notisi ya kumuongeza shahidi wa ziada Betha Mamuya ambaye ni muhimu kwani ndiye aliyefanya uchunguzi wa dawa za kulevya na kufunga dawa hizo.
Ombi hilo lilipingwa na mawakili wa utetezi wakiongozwa na Yassin Memba kwa madai kwamba, hakuna sababu za msingi za kuahirishwa usikilizwaji wa shauri hilo na kwamba kwa kuwa upande wa Jamhuri ulidai una mashahidi wawili hivyo waendelee.
Memba alidai hakuna sheria inayoelekeza shahidi fulani asitoe ushahidi kabla ya mwingine. Kutokana na hali hiyo, Jaji Grace aliamua kuahirisha shauri hilo hadi jana kwa kutoa uamuzi.
Katika uamuzi wake jana, Jaji Grace alikubaliana na ombi la upande wa Jamhuri la kuahirisha shauri hilo ili shahidi Betha awe wa kwanza kutoa shahidi.
Baada ya kutolewa uamuzi huo, Wakili Mwangamila alidai waliwasilisha hati ya kuitwa kwa mashahidi wa ziada Betha na Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP)  Neema ili aende utoa ushahidi kwa madai kuwa Betha ni shahidi wa msingi kuanza kutoa ushahidi wake.
Hata hivyo, mawakili wa utetezi walipinga kauli ya upande wa Jamhuri kwa madai kuwa juzi walieleza wanatarajia kumuita Betha, lakini ndani ya dakika chache kabla ya kutolewa uamuzi, walipewa notisi ambayo imetaja jina la mtu mpya ambaye ni ASP, Neema.
Wakili Evod Mmanda, alidai wamepewa notisi hiyo muda mfupi kabla ya kuingia mahakamani na upande wa Jamhuri uliwasilisha notisi hiyo kabla ya kutolewa uamuzi.
"Jana (juzi), upande wa Jamhuri uliomba ahirisho ili uweze kupata nafasi ya kuwasilisha notisi mahakamani ya kumuita shahidi wa ziada Betha Mamuya. Ina maana notisi ilitakiwa iwasilishwe leo (jana), baada ya kutolewa uamuzi. Kwa maana hiyo kisheria hakuna notisi mahakamani. Notisi halali ni ile itakayowasilishwa baada ya uamuzi," alidai Mmanda.
Alidai hakuna notisi ya kuita mashahidi wa ziada na kama mahakama itaona ni notisi basi ione upande wa utetezi wamepewa wakati ambao si muafaka.
Naye Wakili Johnson Jamhuri alidai akiwa wakili wa utetezi hajakabidhiwa notisi hiyo, hivyo kunaonyesha haipo.
Akijibu hoja za mawakili hao, Wakili Mwangamila akishirikiana na Wakili wa Serikali Hamidu Mwanga, walidai jukumu la kukabidhi upande wowote nyaraka kutoka mahakamani katika kesi za jinai si la kwao ni la wahudumu wa mahakama.
Kuhusu uhalali wa notisi, Mwangamila alidai upande wa utetezi unajichanganya kwa kauli zao, hivyo aliiomba mahakama kuiona notisi hiyo imeletwa kwa wakati muafaka.
Baada ya kusikiliza malumbano ya kisheria, Jaji Grace alisema atatoa uamuzi mdogo keshokutwa na kuamuru washitakiwa kurejeshwa rumande.
Wakati washitakiwa wakitolewa mahakamani kupelekwa mahabusu walikuwa wamejifunika vitambaa kichwani kuficha
sura zao kukwepa kupigwa picha, ambapo mmoja wao alijaribu kutaka kumpiga mpigapicha.

Ilboru yafungwa kufuatia jaribio la kuichoma moto


NA LILIAN JOEL, ARUSHA
SHULE ya sekondari ya vipaji maalum ya Ilboru iliyoko wilayani Arumeru mkoani hapa, imefungwa kwa muda usiojulikana baada ya kutokea kwa tukio la jaribio la kuichoma moto.
Tangazo la kufunga shule hiyo lilitolewa ghafla jana asubuhi na Mkuu wa Shule, Julius Shila baada ya kushauriana na bodi ya shule.
Askari polisi wenye sare na waliokuwa kiraia, walionekana wakifanya doria katika eneo la shule na viunga vyake katika harakati za uchunguzi wa awali kubaini chanzo na wahusika wa jaribo la kuchoma moto shule hiyo yenye sifa ya kutoa viongozi wengi wa kitaifa.
Pamoja na kufunga shule, wanafunzi 10 wamesimamishwa masomo kwa siku 21, huku wenzao wanne wakiwa wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano.
Kwa mujibu wa tangazo hilo, wanafunzi wote watatakiwa kurejea shuleni hapo baada ya kudahiliwa na wakuu wa wilaya zao.
Katikati ya hofu hiyo, wanafunzi waliohojiwa na mwandishi wa habari hii wakiwa wanarudi makwao, waliwahusisha baadhi ya walimu chuoni hapo na sakata la kutaka kuchoma shule hiyo.
Walidai kuwa vitisho vya kuchomwa moto kwa shule hiyo vilianza mwaka jana, ingawa polisi walifanya uchunguzi, lakini hakuna taarifa zaidi zilizotolewa.
Walisema wiki iliyopita kulikuwa na harufu ya mafuta ya petroli yaliyomwagwa eneo jirani na bweni la shule, tukio ambalo polisi walithibitisha kuwa kweli.
ìBaadhi ya walimu walikiri kuhusika, mwaka jana walikubali shule ilitaka kuchomwa moto, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa na tukio kama hilo limejitokeza tena wiki iliyopita, sasa tunahofia usalama wetu,î alidai mwanafunzi mmoja wa kidato cha tatu.
Kaimu Ofisa Elimu wa Mkoa, Sifael Mollel, alisema katika uchunguzi wa madai hayo unaendelea katika kipindi hiki ambacho wanafunzi wamepewa likizo.
Alisema kuwepo kwa hofu hiyo na wasiwasi wa kuzuka vurugu ndiko kulikosababisha shule ifungwe kwa muda, licha ya kwamba walikuwa bado hawajamaliza mitihani.
ìUongozi umeamua wanafunzi warudishwe nyumbani kutokana na hofu ya shule kuchomwa moto, wanafunzi walikuwa wakifanya mitihani kabla ya kuanza likizo fupi, lakini kuwepo kwa tishio hilo na kuzuka kwa vurugu, ilionekana ni vema ikafungwa,î alisema.
Alisema kwa kawaida likizo fupi ni ya siku 10, lakini kwa tukio hili wanafunzi hao wamepewa maelekezo ya kwenda kuonana na wakuu wa wilaya zao kwa udahili kabla ya kurejea shuleni.
Akizungumzia vitisho vya moto, alisema wanafunzi hao waliwasilisha barua ofisini kwake wakitoa madai kuwa, baadhi ya walimu walikuwa wanataka kuchoma moto shule hiyo.
Alisema polisi walienda kufanya uchunguzi Ijumaa, ambapo waliona harufu ya petroli iliyokuwa imemwagwa jirani na bweni.
Kaimu ofisa elimu huyo hakutawataja wanafunzi ambao wanahojiwa na polisi wala wanafunzi 10 ambao wamesimamishwa kwa siku 21.
Hata hivyo, Shila alikataa kuzungumza na wanahabari kuhusu matukio hayo na hata alipopigiwa simu, alikuwa akiikata mara baada ya kujitambulisha kuwa ni mwandishi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Liberatus Sabas, alikiri polisi kuwepo shuleni hapo wakati tangazo la kufungwa shule likitolewa, lakini alisema ilitokana na sababu za kulinda usalama.

Magufuli ataka uchunguzi vituo vya mizani


NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli ameagiza kufanyika kwa uchunguzi kuhusu utendaji wa vituo vya mizani mkoani Iringa.
Magufuli alitoa agizo hilo katika ziara yake ya kikazi mkoani humo katika mkutano wa pamoja na wafanyakazi wa taasisi zinazosimamiwa na wizara hiyo.
Alisema hayo wakati akipokea taarifa za utekelezaji wa majukumu ya kila taasisi mkoani humo na ndipo lilipojitokeza suala la tozo iliyokusanywa kwa magari yaliyokamatwa yakiwa yamezidisha uzito kwa kipindi cha Julai, mwaka huu, katika kituo cha mizani cha Wenda kilichopo kati ya Iringa na Ifunda.
Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Iringa, Injinia Poul Lyakurwa, alimtaarifu Waziri Magufuli kuwa kiasi cha sh. milioni 31.9 kilikusanywa katika kipindi hicho.
Waziri huyo alishtushwa na kiwango hicho kilichosomwa katika taarifa kuwa kimetokana na magari 735 yaliyokamatwa kati ya magari 20,700 yaliyopimwa sawa na asiliamia 3.5.
ìTakwimu hizi sizikubali, kwani wastani wa magari yanayokamatwa katika nchi nzima unakaribia asilimia 40, iweje barabara kuu kama hii iwe na kiwango kidogo kiasi hicho cha magari yaliyokutwa na makosa, hapa ni lazima pafanyike uchunguzi, hali hiyo hawezi kuiruhusu hata kidogo kuendelea,” alisema.
Katika hatua nyingine,  Waziri Magufuli alimpongeza meneja huyo kwa kufukuza wafanyakazi 18 katika kituo cha mizani cha Makambako kwa kutokuwa waaminifu katika kazi zao.
Waziri huyo alibainisha kuwa takriban asilimia 70 ya wafanyakazi waliokuwa katika vituo mbalimbali vya mizani katika barabara nchi nzima wamebadilishwa baada ya kukamilika kwa kazi ya  kutangaza nafasi hizo upya.
Alisisitiza kuwa wizara hiyo itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali, zikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB), Jeshi la Polisi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na hata kutumia makondakta na wasaidizi katika magari ya usafirishaji ili kuendelea kubaini mbinu zinazotumika katika vitendo vya rushwa katika vituo vya mizani nchini.
Kwa upande mwingine, Wakala wa Majengo Nchini (TBA) na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), wametakiwa kuwa wabunifu ili waweze kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili

WAZAZI yaambiwa iache kufanya kazi kwa mazoea


NA STEPHEN BALIGEYA, LUSHOTO
MWENYEKITI wa Jumuia ya Wazazi Mkoa wa Tanga, Dk. Edmund Mndolwa, amewataka viongozi wa jumuia hiyo kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wabadilike kulingana na siasa za sasa.
Alisema kuendelea kufikiri kwamba chama ni imara bila kufanya kazi ni kukipa kazi ngumu katika uchaguzi mbalimbali, hivyo wanatakiwa kubuni mbinu mpya na zenye tija kwa chama dhidi ya wapinzani.
Wito huo aliutoa juzi wakati wa ziara yake ya kuwashukuru kwa kumchagua kuwa mwenyekiti wa jumuia hiyo, ambayo anaifanya katika wilaya zote tisa za mkoa huo.
Dk. Mndolwa ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, alisema limekuwa jambo la kawaida kwa wenyeviti na makatibu wa jumuia kufanya kazi zisizoeleweka kwa dhana ya ukubwa wa chama, kitu ambacho kimechangia kukiumiza katika baadhi ya uchaguzi.
Kwa hali hiyo, aliwataka viongozi hao kushuka chini kwa wanachama, kwani huko ndiko kwenye msingi na hazina ya watu wengi ambao ni mtaji wa chama kwa siku nyingi kuliko kukaa ofisini.
“Makatibu acheni kuwa kama miungu watu kwa kutoa maagizo kwa simu, nendeni ngazi za kata na kuona utekelezaji wa ilani yetu unavyosimamiwa na viongozi ngazi ya tawi, ì alieleza Dk.  Mndolwa.
Aidha, aliwaeleza kuwa katika kufanikisha ushindi wa chama katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani na uchaguzi mkuu 2015, lazima makundi yaachwe na wafanye kazi kama timu.
ìHatuwezi kukabiliana na upinzani kwa kuhujumiana, lazima tuwe kitu kimoja tupigane kwa ajili ya chama na sio kwa ajili ya mtu, maana mtu atapita, lakini chama hakiwezi kupita,î alisisitiza.
Pia, alisema makundi hudhoofisha nguvu ya siasa katika chama kwa  kiasi kikubwa, na kutoa nafasi kwa wapinzani kuchukua baadhi ya majimbo, jambo ambalo linapaswa kupigwa vita.

Mkataba kufua umeme mto Kagera watiwa saini


NA ANGELA SEBASTIAN, BUKOBA
MAWAZIRI watatu wa nchi za Afrika Mashariki, wametia saini mikataba miwili inayohusu utekelezaji wa mradi wa kufua umeme wa maji katika mto Kagera.
Mradi huo utajengwa katika eneo la Rusomo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.
Mikataba hiyo, ilitowa saini jana mjini hapa na mawaziri wa nchi za Rwanda, Burundi na Tanzania, katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Magharibi.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alisema kutiwa saini kwa mikataba hiyo kumetengeneza historia mpya, kwani mradi huo ulianzishwa tangu mwaka 1974, lakini ulikwama kutokana na sababu mbalimbalia, ikiwemo ukosefu wa fedha.
Alisema mwaka 2005, mawaziri wa nishati na madini wa nchi hizo walikaa na kujadili jinsi ya kuutekeleza, mazungumzo yakiendelea, huku wakipanga mikakati ya kupata fedha, na kwamba hivi sasa unatarajiwa kuanza rasmi 2015.
Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, mradi huo unatarajiwa kukamilika mwaka 2018, na kwamba uko katika awamu mbili ambapo ya kwanza ni kufunga mtambo wa kufua umeme utakaogharimu dola za Marekani milioni 340 zikiwa ni mkopo kutoka Benki ya Dunia.
Alisema awamu ya pili ni ujenzi wa njia za usafirishaji wa umeme kutoka Rusumo hadi Nyakanazi, Rusumo hadi Kigali na Rusumo hadi Burundi, sambamba na kulipa fidia kwa wananchi walioathiriwa na mradi huo.
Akizungumzia kuhusu mgogoro uliokuwepo juu ya mradi huo kati ya nchi hizo, waziri huyo alisema walijadili suala hilo kwa uwazi, ambapo mwanzo ilibainika ulifanywa na Wanyarwanda tu, ambapo uamuzi wa hivi sasa  kila nchi itatoa asilimia 30 ya wafanyakazi katika kutekeleza mradi huo na asilimia 10 watapewa wafanyakazi kutoka nje ya nchi hizo.
Kwa upande wake Naibu Kamishna Msaidizi wa Nishati ya Umeme nchini, Innocent Luoga, alisema mradi huo unaratajiwa kuzalisha megawati 80, ambapo kila nchi itapata megawati 27.
Waziri wa Miundombinu wa Rwanda, Profesa Silas Rwakabamba na Waziri wa Nishati wa Burundi, Manirakiza Cíome, walisema mradi huo umekuja kwa wakati muafaka na itakuwa chachu ya maendeleo ya uchumi wa nchi hizo, kwani utaongeza pato kwa wananchi.

Wananchi asilimia 96 wapata majisafi


NA MWANDISHI WETU, MBEYA
MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jiji la Mbeya, imeongeza uzalishaji wa maji kutoka mita za ujazo 32,000 kwa siku hadi mita za ujazo 50,000.
Hali hiyo imesababisha upatikanaji wa maji ya kutosha ambapo asilimia 96 ya wananchi wanapata maji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo, Injinia Simeon Shauri, aliyasema hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro, wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya mamlaka hiyo.
Shauri alisema mamlaka imeweza kujiendesha kibiashara kwa kujitegemea na uwezo huo umetokana na kukamilika kwa miradi ya maji na usafi wa mazingira ya awamu ya kwanza na ya pili.
ìWateja wa majisafi wameongezeka kutoka 24,388 hadi wateja 34,242, na kwa upande wa majitaka wameongezeka kutoka wateja 379 hadi 1,261 kwa sasa,î alisema.
Alisema huduma imeboreshwa kutoka wastani wa saa 21 kwa siku hadi saa 23 kwa siku, ambapo asilimia 78 ya wateja wanapata maji saa 24 kwa siku.
Mkurugenzi huyo alisema mahitaji halisi ya maji mjini hapa kwa sasa ni wastani wa mita za ujazo 42,000 kwa siku, hata hivyo, wakati wa kiangazi hupanda hadi mita za ujazo 46,000 kwa siku na hiyo hutokea Agosti, Septemba na Oktoba.
Alisema mamlaka inavyo jumla ya vyanzo 13 vya maji, ambavyo kwa jumla hutoa mita za ujazo 50,000 kwa siku, huku vyanzo hivyo vikiwa na mitambo 10 ya kusafisha na kutibu maji.
Kwa mujibu wa Injinia Shauri, mitambo hiyo ipo katika maeneo ya Swaya, Imeta, Sisimba, Lunji, Mwatezi, Iduda, Nzovwe, Iyela, Nsalaga na Nelotia.
Naye, Kandoro alisema mamlaka hiyo imeendelea kujitegemea na kuwapongeza wajumbe wa bodi iliyomaliza muda wake chini ya Dk. Grant Mwakatundu kwa kuweza kuisaidia mamlaka kuweza kutoa huduma stahili kwa wakazi wa jijini hapa.
Kandoro aliwataka wajumbe waliomaliza muda wao kushirikiana na bodi mpya ambayo itaongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya, Atuganile Ngwala, kutokana na kuwa na  uzoefu.

Chagua jibu sahihi katika hisabati yamkera waziri


NA SOLOMON MWANSELE, MBEYA
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema ufaulu wa somo la hisabati katika shule za msingi na sekondari nchini hauridhishi.
Amesema mustakabali wa taifa unawataka wadau wote kuunganisha nguvu ili kukabiliana kikamilifu na changamoto hiyo.
Dk. Mwakyembe alitoa rai hiyo wakati wa ufunguzi wa semina ya hisabati na mkutano wa kitaifa wa mwaka wa 48 wa Chama cha Hisabati Tanzania, unaofanyika Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU), mjini hapa.
Alisema matokeo ya somo la hisabati kitaifa ni changamoto kubwa, na kwamba serikali itaendelea kukiunga mkono chama hicho katika kuhakikisha kinafanikiwa kutimiza malengo yake ya kuinua somo hilo nchini.
Aidha, waziri alisema serikali itahakikisha kuwa walimu wengi zaidi wanahudhuria mikutano ya chama hicho na siyo kama ilivyo sasa, ambapo mahudhurio hayaridhishi.
ìHuu ndio mzaha uliopo katika utendaji wetu wa kaziÖ ni lazima walimu wote waliokuwa wamepewa taarifa za semina na mkutano huu kisha hawajahudhuria wajieleze walikuwa wapi. Hatuwezi kuendelea kuifumbia macho hali hii,î alisisitiza.
Alisema  atahakikisha analifikisha suala hilo kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, kuhusu hali hiyo ili hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya wahusika.
îImekuwa ëbusiness as usuallyí na hili nawaahidi kuwa nitalifikisha mbele zaidi kwa waziri husika, ili kila aliyepewa mwaliko, lakini hajafika atueleze alikuwa wapi, kama alikuwa amempeleka mkewe kusuka, atueleze,” alisema.
Waziri alisema anaungana na chama hicho kupinga mfumo wa kuchagua jibu sahihi katika mitihani ya hisabati kwa shule za msingi, kwani haiwajengi wanafunzi kufikiri.
Alikiri ni vyema mfumo huo uachwe kutumiwa na wanafunzi wa shule za msingi, bali uendelee kwa shule za sekondari ili watoto wa shule za msingi wajifunze somo hilo kwa ufasaha zaidi na siyo kupitia mfumo huo wa kuchagua.
Dk. Mwakyembe alisema kwa hali ilivyo, bado siyo sahihi kwa mfumo huo kutumika kwa shule za msingi, hivyo ni lazima kwanza mtoto aanze kujengewa msingi imara wa somo hilo tangu akiwa shule ya msingi.

Saturday 14 September 2013

Padri amwagiwa tindikali Zanzibar


NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR
PADRI wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mpendae, Zanzibar, Anselmo Wan'gamba, amemwagiwa tindikali usoni na watu wasiojulikana.
Tukio hilo lilitokea jana, saa 10.30 jioni, eneo la Mlandege wakati akitoka kupata huduma ya mawasiliano ya internet.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba, wanaendelea na uchunguzi wa kina ambao tayari umeanza.
Padri Mwang'amba ni Mkuu wa Kituo cha Malezi cha Vijana kilichopo Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, ambacho kinatunza vijana kwa ajili ya kuwapatia mafunzo mbalimbali.
Mkadam alisema walipokea taarifa hiyo na wanafanya uchunguzi ili kufahamu mtandao wa watu wanaojihusisha na uhalifu huo.
Kwa upande wake, Daktari wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, ambaye alimpokea padri huyo hospitalini hapo, Abdalla Haidari, alisema kiongizi huyo wa dini ameumua usoni na kifuani.
Alisema padri huyo amejeruhiwa na kwamba baada ya kumfanyia uchunguzi waligundua kuwa amemwagiwa tindikali.
Dk. Haidari alisema katika maelezo ya padri huyo, alishambuliwa na watu ambao hakuwafahamu wakati akitokea Sunshine, Mlandege.
Alisema wakati anatoka kupata huduma hiyo alimwagiwa maji aliyohisi tindikali na kukimbilia hospitalini hapo.
Naye mfanyakazi wa internet hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Salama, alikiri padri huyo kufika na kupata huduma hiyo na kuondoka, lakini alishangaa kumuona akirudi huku akilalamika kufanyiwa kitendo hicho.
Mei 23, mwaka huu, Sheha wa Shehia ya Tomondo, Wilaya ya Magharibi Unguja, Mohammed Omar Said (65), alimwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana alipokuwa akichota maji nje ya nyumba yake majira ya saa 2:45, usiku.
Tukio lingine ni lile la Agosti 9, mwaka huu, ambalo lilidaiwa kufanywa na watu wawili waliokuwa kwenye pikipiki maarufu kama Vespa, mjini Zanzibar, ambapo raia wawili wa Uingereza, Kate Gee (18) na Kristie Trup (18) walimwagiwa tindikali.
Tukio hilo lilitokea lilitokea saa moja usiku wakati raia hao walipokuwa wakitoka kunywa kahawa katika Baraza la Jaws Corener, mjini humo.
Pia, Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Fadhili Soraga, alifanyiwa unyama huo Desemba, mwaka jana na mtu asiyefahamika wakati akifanya mazoezi.



Wednesday 11 September 2013

Kashfa ya kigogo


Na Mwandishi Wetu
UFISADI mkubwa umebainika ndani ya Bodi ya Tumbaku, baada ya Mkurugenzi Mtendaji wake, Wilfred Mushi, kudaiwa kujilipa mshahara na posho mbalimbali kinyume na utaratibu.
Mbali na kujilipa mshahara na posho mbalimbali, ambazo zimepitishwa na Bodi, Mushi anajilipia posho ya pango la nyumba kwa dola za Marekani 1,200, (sh. 1,920,000), tofauti na serikali iliyomtaka aishi katika nyumba yenye gharama ya sh. 400,000.
Uhuru ilifanikiwa kupata nyaraka mbalimbali zilizoonyesha malipo anayojilipa mkurugenzi huyo, ambapo pia anadaiwa kujinunulia samani za ndani vikiwemo vitanda na makochi kwa sh.milioni 23, kinyume na utaratibu.
Pia, nyaraka hizo zinaonyesha kila afanyapo safari kutoka Dar es Salaam kwenda Tabora, hujilipa sh. milioni 2.8 kiasi ambacho ni kikubwa ikilinganisha na kile anachostahili licha ya kupatiwa posho ya mafuta na dereva.
Chanzo chetu cha habari, kilidai kuwa mkurugenzi huyo pia hujilipa sh. milioni tatu kila mwezi kama mshahara, kiwango ambacho bodio hakikitambui.
Kilisema mshahara halali wa bosi huyo ni sh. milioni 2.9, ambazo nazo huzichukua na kufanya kila mwezi awe anajilipa kiasi cha milioni 5.9 kinyume na utaratibu wa ambao Bodi ya Tumbaku imemuidhinishia.
Taarifa zaidi zilidai kuwa Mushi anajilipa sh. milioni 2.7 kama gharama za simu, ambapo alitakiwa kulipwa sh. 400,000 kama malipo stahili kwa huduma ya mawasiliano kila mwezi.
Alipoulizwa kuhusiana na kashfa hiyo jana alipozungumza na Uhuru, Mushi, alisema kila bodi ya mazao ina utaratibu wake inaoufuata kisheria kutokana na uendeshaji wake kujitegemea.
Alisema viwango vya fedha hizo anazojilipa ni haki yake kisheria na zilipitishwa kihalali na bodi.
“Hizo taarifa hazina ukweli na nyaraka zilizopo sizijui kuhusiana na malipo wanayodai, ila nachojua nalipwa sahihi na kama mnahitaji taarifa zaidi, njooni ofisini kwangu Morogoro,” alisema.
Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Vita Kawawa, ambaye pia ni Mbunge wa Namtumbo (CCM), alikiri kupitisha malipo hayo na kusema kuwa  mkurugenzi huyo anastahili kulipwa fedha hizo.
“Huo si ufisadi, ni kweli tumemuidhinishia na lazima alipwe kama wakurugenzi wa bodi zingine na hata malipo ya nyumba ni stahili yake kwa kuwa nyumba aliyokuwa anaishi haiendani na hadhi yake,” alisema.
Vita, alisema watu kama hao lazima walipwe hasa ikizingatiwa kuwapata watumishi wa namna hiyo wanaoongoza bodi za mazao ni jambo gumu na yuko tayari kumtetea.
Alidai kuwa matatizo yanayojitokeza sasa yanalenga kumpiga vita mwenyekiti huyo kutoka kwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika nchini.
Alisema Mushi alikuwa miongoni mwa wajumbe wa tume iliyoundwa na serikali kuchunguza ufisadi katika Chama cha Ushirika mkoa wa Tabora.
Hata hivyo, Vita, alisema malipo wanayolalamikia juu ya Mushi, alikuwa analipwa pia mkurugenzi aliyemtangulia.
Habari zilizopatikana kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, zilisema mkurugenzi wa bodi hiyo anapaswa kulipwa mshahara wa sh. milioni 2.9 na uamuzi wa Bodi unatoa tafsiri tofauti juu ya malipo halisi ya Mushi.

000

JK awatangazia kiama ‘mchwa’



NA PETER KATULANDA, MWANZA
RAIS Jakaya Kikwete amehitimisha ziara yake mkoani hapa na kuwaangazia kiama watendaji wa halmashauri watakaochakachua fedha za ujenzi wa nyumba za walimu.
Aliwasisitiza wananchi kuwa maisha bora hayaji kwa kudondoshewa fedha na wanaotafuta ‘kuhomola’ (kula) kupitia kwa wakulima.
Alisema wengi wao huchakachua fedha hizo kupitia kwenye kilimo cha mkataba, wakiwemo wanasiasa.
Rais Kikwete, alisisitiza kuwa ahadi yake ya kujenga meli na kuboresha huduma za usafiri katika Ziwa Victoria na mengine, si hewa, meli mbili mbadala wa MV Bukoba, zitajengwa.
Alisema hayo jana alipokuwa akihitimisha ziara yake ya siku tano mkoani hapa, kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam.
Alizungumza na viongozi mbalimbali wa Chama na serikali kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza, wazee maarufu na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini.
Alisema dhamira ya serikali ni kuinua hali za watu katika sura mbili, kuwapa huduma za kiuchumi na kijamii kwa huduma bora ikiwemo maji, umeme, elimu, miundombinu ya usafiri, zahanati na kuwajengea mazingira ya ajira na maendeleo.
Pamoja na dhamira hiyo, Rais Kikwete hakuona mahali popote katika ziara hiyo ambapo wanajishughulisha na maendeleo ya viwanda wakati ni moja ya njia za kujenga uchumi na kukuza ajira.
Alisema kuendelea kuwa na miji ambayo haina viwanda ni matatizo.
“Kuna wengine wamebeba dhana potofu, wanasema maisha bora yako wapi, sisi hatukusema tutagawa pesa…unashinda kwenye pulu, fedha hazitadondoka kwenye toka huko na kuingia mfukoni mwako, ” alisema.
Pamoja na kupongeza jitihada za kilimo, Rais Kikwete alisema kuna hali ya kutoelewana katika kilimo cha mkataba.
Alisema baadhi ya watu wakiwemo wanasiasa, wanataka kujinufaisha kwa kukipiga vita kilimo hicho, wakati kinamnufaisha mkulima.
Kutokana na hilo, aliuagiza mkoa ukae na wadau wajadili na kupata ufumbuzi wa kilimo hicho.
“Watu wanataka kuhomola tu, tafuteni kwa kula kwingine si kwa wakulima, watu hawataondokana na umaskini kwa kulima mazao ya chakula tu, ambayo hawawezi kuyapandisha bei.
“Wataondokana na mazao ya biashara, nimeona zao la dengu linakubali, lifanyeni kuwa la biashara,” alisema na kuiagiza serikali mkoani hapa ijipange kuhamasisha zao hilo.
Alipongeza jitihada zifanywazo katika sekta ya elimu mkoani humo, na kuwaonya watendaji wa halmashauri za wilaya kutumia fedha za ujenzi wa nyumba za walimu vizuri na wasitafute makandarasi wezi ambao watashirikiana nao kuzichakachua.
Alisema kiongozi mzuri ni yule anayeonea fahari maendeleo ya wananchi wake. Alisema kila halmashauri imepewa sh. milioni 500.
Rais alizungumizia pia njia mbadala ya kuboresha na kujenga reli ya kisasa itakayoweza kuchukua mabehewa mengi.
“Kwenye ziwa shabaha yetu ni kuboresha usafiri, ..Ukerewe kumekuwa na malalamiko ya meli ya Butiama kuwa haitoi huduma sawa sawa, tutalishughulikia, tuliahidi kujenga meli mpya taratibu zinaenda vizuri, mambo yakikaa sawa, tutajenga meli kubwa mbili badala ya Mv Bukoba,” alisema Rais Kikwete.
Hata hivyo, alisema hakufurahishwa na kasi ya uboreshaji wa huduma za afya na kwamba, atakutana na watendaji wa Bohari ya Dawa (MSD) na kuangalia matatizo yaliyopo ili waondoe tatizo la upungufu wa dawa katika hospitali mbalimbali mkoani hapa.

Kinana atoa somo kwa wamiliki migodi


NA SULEIMAN JONGO, KAHAMA  
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amewataka wawekezaji nchini hasa wa migodi ya madini, kutoa kipaumbele kwa jamii inayowazunguka pindi wanapotaka kuchangia miradi ya maendeleo.
Kinana aliyasema hayo juzi wakati akikagua ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Mwendakulima, wilaya ya Kahama, Shinyanga, akiwa katika ziara ya kikazi kwenye mikoa mitatu ya kanda ya ziwa.
Alisema ili kuhakikisha wananchi hasa walio kwenye maeneo ya uwekezaji wa miradi mbalimbali, wanapaswa kuacha kiasi kikubwa cha fedha walizozitenga kwa ajili ya kushiriki maendeleo ya taifa. 
“Kwa mfano hapa Kahama, wapo wawekezaji wanaochimba madini, ni vyema wakashiriki kikamilifu kwa kuacha asilimia 90 ya bajeti yao ya kuchangia miradi ya maendeleo badala ya kupeleka katika maeneo mengine kwa ajili ya kuwafurahisha viongozi,” alisema Kinana.   
Kwa mujibu wa Kinana, endapo wawekezaji watazingatia hilo, wataondoa mgogoro kati yao na wananchi kwa kuwa wataona manufaa ya moja kwa moja yanayotakana na rasilimali zao.     
Kwa upande wake, Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, aliwataka wananchi kuwa karibu na mchakato wa katiba mpya ili kuwabaini watu wanaotaka kupenyeza maslahi yao binafsi kwa lengo la kuuharibu mchakato huo.   
Nape, alisema wananchi wana nafasi kubwa katika kuhakikisha mchakato huo unafanikiwa na hatimaye kupatikana kwa katiba ya Watanzania wote. 
“Fuatilieni mchakato wa katiba mpya kwa karibu, kwa kuwa wapo baadhi ya watu hasa kutoka vyama vya upinzani kikiwemo CHADEMA, ambao kwa makusudi wanataka kuharibu mchakato huu kwa maslahi wanayoyajua wao. 
Nape na Kinana, wako kwenye ziara ya wiki tatu katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara, ambako watatembelea wilaya zote kuhamasisha maendeleo ya jamii.  

Utulivu watawala mitihani la Saba


Na Mohammed Issa
WANAFUNZI wanaomaliza elimu ya msingi, jana walianza kufanya mitihani yao huku hali ya utulivu ikiwa imetawala kwenye vituo vingi mkoani Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, wanafunzi 868,030, wamesajiliwa kufanya mtihani huo Tanzania Bara, kati yao wavulana ni 412,105, sawa na asilimia 47.47 na wasichana ni 455,925, sawa na asilimia 52.52.
Uhuru, ilitembelea baadhi ya shule katika mkoani Dar es Salaam na kushuhudia wanafunzi wakifanya mitihani yao kwa utulivu na ulinzi ukiwa umeimarishwa.
Akizungumza kwa njia ya simu jana, msemaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ntambi Bunyanzo, alisema Waziri wa wizara hiyo, Dk.Shukuru Kawambwa, alitembelea baadhi ya shule kujionea hali halisi katika mkoa wa Dar es Salaam.
Alisema Dk.Kawambwa, alitembelea shule ya msingi Kimara Baruti, Mbezi na kwamba, lengo la ziara hiyo alitaka kujionea namna usimamizi na ulinzi ulivyoimarishwa.
Bunyanzo, alisema kwenye maeneo yote nchini, mitihani inafanywa katika hali ya utulivu na hakuna taarifa zozote mbaya zilizoripotiwa. Masomo yanayofanyiwa mtihani ni pamoja na Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii.
Katika shule za msingi Kijitonyama, Ilala Boma, Kigogo, Ali Hassan Mwinyi, Makumbusho na Mnazi Mmoja, hali ya utulivu ilitawala na ulinzi uliimarishwa.

Rufani ya Lissu kusikilizwa leo


Na Mwandishi Wetu, Dodoma
JOPO la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani Tanzania, kesho litaanza kusikiliza rufani dhidi ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, (CHADEMA).
Kwa mujibu wa ratiba za vikao vya mahakama hiyo, rufani hiyo itasikilizwa na Jopo la Majaji Salum Massati, Engela Kileo na Natalia Kimaro.
Rufani hiyo iliyokatwa na Shaaban Seleman na wenzake wawili dhidi ya Lissu, itaanza kusikilizwa saa tatu asubuhi.
Seleman na wenzake, walikata rufani kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, ambayo ilitupilia mbali kesi ya uchaguzi waliyoifungua kupinga ushindi wa Lissu.
Hata hivyo, kabla ya kuanza kusikilizwa kwa rufani hiyo, jopo hilo la majaji linatarajiwa kusikiliza pingamizi zilizotolewa na upande wa wajibu rufani (Lissu).
Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma jana, Lissu, alisema wakati wa usikilizwaji wa rufani hiyo, atawasilisha hoja saba za kuipinga.