Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Pata mafanikio, tangaza hapa

Tangaza nasi hapa.

Sunday 17 May 2015

Uwanja wa ndege wa shambuliwa



KABUL, Afghanistan
WATU watatu wamefariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko katika uwanja wa ndege wa kimataifa uliopo mjini Kabul.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema mtu mmoja alijitoa mhanga kwa kujilipua ambapo aliwalenga wanajeshi wa kimataifa nje ya lango kuu la uwanja huo.
Lango hilo hutumiwa na vikosi vya kijeshi vya kigeni, ambapo bado haijabainika endapo walinusurika na shambulio hilo.
Msemaji wa polisi alisema, shambulio hilo lilifanyika karibu na ofisi za safari za ndege nchini humo zilizoko nje ya uwanja.
Shambulizi hilo linafanyika ikiwa ni siku tatu baada ya mwanamgambo mmoja kuwaua watu 14 wakiwemo raia tisa wa kigeni mjini humo.

Nkuruzinza aonya





RAIS Pierre Nkuruzinza, ametoa onyo kali kuhusiana na jaribio lingine lolote la kutaka kuchukua madaraka ya nchi hiyo kwa kutumia nguvu.
Alisema jaribio la namna hiyo halipaswi kufanyika tena na serikali itahakikisha inakabiliana na makundi yenye nia ya kuvuruga amani kwa kuwa vitendo hivyo vitasababisha umasikini na vita.
Nkuruzinza alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku mbili baada ya Marekani kumuonya kutoendelea na nia ya kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Marekani imesema kitendo cha Nkuruzinza kugombea tena urais, kitazorotesha usalama nchini humo na kutishia misaada ya kimataifa.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jeff Rathke, alisema nchi hiyo inawasiwasi kufuatia uwezekano wa kutokea ghasia zaidi baada ya Nkurunziza kurejea Burundi.
Alisema Marekani inamtambua Nkurunzinza kama rais halali wa Burundi licha ya kusisitiza kiongozi huyo kutowania muhula wa tatu.
Baadhi ya maofisa wa kijeshi walioshiriki kuongoza mapinduzi wamekamatwa huku wengine wakitokomea na kusakwa na majeshi watiifu wa serikali.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Generali Godefroid Niyombare, anaendelea kusakwa

Wakimbizi wa Burundi wahifadhiwa Lake Tanganyika



KUFUATIWA kuongezeka kwa idadi ya wakimbizi kutoka Burundi, uwanja wa michezo wa Lake Tanganyika, umetumika kwa muda kuhifadhia wakimbizi wakati wakipatiwa msaada wa chanjo na matibabu.
Kwa mujibu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la UNHCR, idadi ya watu 100,000 wamekimbia nchini Burundi kufuatia mzozo wa kisiasa unaoendelea.
Idadi kubwa ya wakimbizi hao wamepokelewa nchini Tanzania huku wengine wakikimbilia nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Rwanda na Uganda. Msemaji wa UNHCR mjini Geneva, Karin de Gruijl alisema idadi imeongezeka zaidi siku chache zilizopita huku wengine wakiishi kwenye fukwe za Ziwa Tanganyika.
Alisema kufuati hali hiyo, wengine wamehifadhiwa kwa muda kwenye uwanja wa Lake Tanganyika kwa ajili ya chanjo, ukaguzi na baadae watapelekwa kwenye kambi za wakimbizi.
Alisema malori 17, yaliyobeba vifaa muhimu kama vile vyandarua dawa na mahema yanapelekwa Kigoma.

Wanaume “vicheko” Kenya



WANAUME nchini hapa wamepokea kwa furaha kusainiwa kwa sheria itakayokabiliana na vitendo vya unyanyasaji hususan majumbani.
Sheria hiyo iliyosainiwa na wiki iliyopita na rais Uhuru Kenyata, inatarajiwa kuwapa ahuweni wanaume waliokuwa wakipigwa na wake zao na kushindwa kuripoti matukio hayo polisi.
Matukio ya wanaume nchini Kenya kupigwa na wake zao yamezidi kuongezeka na kuhatarisha amani katika familia.
Baadhi ya wanaume walisema wamekuwa wakipigwa na wake zao mara kwa mara na kuwafanya kutokua na amani kwenye ndoa zao.
Walisema kinga hiyo ya kisheria itakuwa ni fundisho kwa wanawake wenye kuendekeza tabia za kuwapiga kwa kudai kuwa wameshindwa kutimiza mahitaji ya ndoa na familia madai ambayo wameyakataa.
Kukithiri kwa matukio hayo kunasababisha kuanzishwa chama cha kutetea haki za wanaume na kutaka kuitishwa kwa mgomo wa wanaume kwenye ndoa mpaka sheria hiyo itakapopitishwa.
Mmoja wa waathirika wa vipigo hivyo ni Simon Kiguta, ambaye alipigwa na kujeruhiwa vibaya na mkewe ambapo tukio hilo liliamsha hasira za wanaume wengi nchini hapa.

HABARI ZA MICHEZO KIMATAIFA


Van Gaal aiponda Chelsea

 LICHA ya Chelsea kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England msimu huu, Kocha Mkuu wa Manchester United Louis van Gaal, amesema Arsenal ina kiwango bora zaidi kuliko Chelsea. 


Van Gaal alisema kikosi cha Arsenal kiliweza kuonyesha kandanda safi huku wachezaji wake wakiwa katika kiwango cha juu tofauti na Chelsea.


Kocha huyo alisema Chelsea imetwaa ubingwa huo kwa bahati na iliweza kuzichanga karata zake katika safu ya ushambuliaji na kumalizia vyema mipira na ndio maana iliweza kuvuna pointi nyingi.


Alisema kwa upande wa Arsenal wao ndio walioongoza kwa kuonyesha kandanda safi na la kuvutia lakini iliteleza kwa kufanya makosa madogo madogo ambayo ndiyo yaliyoigharimu timu hiyo.


"Naweza kusema kuwa Arsenal ndio timu bora msimu na hakuna ubishi katika hilo licha ya Chelsea kutwaa ubingwa, " alisema Van Gaal.


Kocha huyo alisema kuna haja sasa ya kujipanga vyema kwa ajili ya msimu ujao ili kikosi chake na timu nyingine ziweze kufanya vyema katika ligi.


Mourinho amwagia sifa Terry

KOCHA wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya England  Jose Mourinho, amesema bila ushawishi wake John Terry asingekuwa katika kikosi hicho.
Mourinho alisema katika kipindi kirefu ameweza kumshawishi Terry kuendelea kuichezea timu hiyo licha ya kutaka kuondoka mara kwa mara.Kocha huyo alisema kila Terry alivyotaka kuondoka alimzuia kwani alikuwa muhimu sana katika kikosi chake na ndio maana alikuwa akimzuia."Nimekuwa nikimzuia Terry kuondoka kwa kuwa mimi kama kocha najua umuhimu wake kwani ameweza kuisaidia sana timu," alisema Mourinho.Alisema mchezaji huyo pamoja na wenzake wameweza kushirikiana vyema na kuiwezesha timu yake kunyakua ubingwa msimu huu.Terry mwenye umri wa miaka 34, ameweza kuichezea Chelsea  mechi za msimu mzima kwa kipindi cha dakika 90.


Kocha Newcastle alia na kiwango




KOCHA Mkuu wa Newcastle John Carver, amesema amesikitishwa na kiwango kilichoonyeshwa na timu yake katika mchezo wa Ligi Kuu England.Katika mchezo huo, Newcastle ilipokea kipigo cha mabao 2-1, dhidi ya QPR.Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Carver alisema timu ilipoteza mchezo huo baada ya kucheza chini ya kiwango.

Carver alisema timu yake ingeweza kushinda lakini safu ya ulinzi ilimuangusha baada ya kukosa umakini na kuruhusu wapinzani wao kupenya na kupata mabao.

"Timu yangu ilicheza chini ya kiwango hali ambayo imesababisha kupoteza mchezo wetu dhidi ya QPL lakini matokeo hayo hayatatukatisha tamaa," alisema Carver.

Kutokana na matokeo hayo, Newcastle inashika nafasi ya nne kutoka mkiani baada ya kujikusanyia pointi 34 wakati QPR ipo nafasi ya pili mkiani ikiwa na pointi 30.

Rodgers:Hakuna kama Gerrard





KOCHA wa Mkuu wa Liverpool, Brendan Rodgers, amesema hakuna mchezaji anayeweza kuchukua nafasi ya nahodha Steven Gerrard.

Rodgers alisema kuondoka kwa Gerrard katika kikosi hicho ni pengo kubwa kwa kuwa nahodha huyo alikuwa hodari na mtu aliyejituma.

Kocha huyo alisema mchezaji huyo alikuwa ni moja ya wachezaji ambao wameisaidia Liverpool kupata mafanikio makubwa.

"Kuna wachezaji wengi na wazuri England, lakini  Liverpool haiwezi kupata mchezaji mzuri kama Gerrard ambaye hawezi kufananishwa na mchezaji yeyote kutokana na mchango wake," alisema Rodgers.

Nyota huyo aliagwa juzi katika mchezo wake wa mwisho ambapo Liverpool ilikubali kipigo cha mabao 3-1, katika mchezo uliopigwa katika dimba la Anfield.

Mchezaji huyo alijiunga na klabu hiyo miaka 17 iliyopita na msimu ujao atavaa jezi ya LA Galax