Sunday 17 May 2015

HABARI ZA MICHEZO KIMATAIFA


Van Gaal aiponda Chelsea

 LICHA ya Chelsea kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England msimu huu, Kocha Mkuu wa Manchester United Louis van Gaal, amesema Arsenal ina kiwango bora zaidi kuliko Chelsea. 


Van Gaal alisema kikosi cha Arsenal kiliweza kuonyesha kandanda safi huku wachezaji wake wakiwa katika kiwango cha juu tofauti na Chelsea.


Kocha huyo alisema Chelsea imetwaa ubingwa huo kwa bahati na iliweza kuzichanga karata zake katika safu ya ushambuliaji na kumalizia vyema mipira na ndio maana iliweza kuvuna pointi nyingi.


Alisema kwa upande wa Arsenal wao ndio walioongoza kwa kuonyesha kandanda safi na la kuvutia lakini iliteleza kwa kufanya makosa madogo madogo ambayo ndiyo yaliyoigharimu timu hiyo.


"Naweza kusema kuwa Arsenal ndio timu bora msimu na hakuna ubishi katika hilo licha ya Chelsea kutwaa ubingwa, " alisema Van Gaal.


Kocha huyo alisema kuna haja sasa ya kujipanga vyema kwa ajili ya msimu ujao ili kikosi chake na timu nyingine ziweze kufanya vyema katika ligi.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru