Sunday 17 May 2015

Mourinho amwagia sifa Terry

KOCHA wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya England  Jose Mourinho, amesema bila ushawishi wake John Terry asingekuwa katika kikosi hicho.
Mourinho alisema katika kipindi kirefu ameweza kumshawishi Terry kuendelea kuichezea timu hiyo licha ya kutaka kuondoka mara kwa mara.Kocha huyo alisema kila Terry alivyotaka kuondoka alimzuia kwani alikuwa muhimu sana katika kikosi chake na ndio maana alikuwa akimzuia."Nimekuwa nikimzuia Terry kuondoka kwa kuwa mimi kama kocha najua umuhimu wake kwani ameweza kuisaidia sana timu," alisema Mourinho.Alisema mchezaji huyo pamoja na wenzake wameweza kushirikiana vyema na kuiwezesha timu yake kunyakua ubingwa msimu huu.Terry mwenye umri wa miaka 34, ameweza kuichezea Chelsea  mechi za msimu mzima kwa kipindi cha dakika 90.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru