Sunday 17 May 2015

Uwanja wa ndege wa shambuliwa



KABUL, Afghanistan

WATU watatu wamefariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko katika uwanja wa ndege wa kimataifa uliopo mjini Kabul.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema mtu mmoja alijitoa mhanga kwa kujilipua ambapo aliwalenga wanajeshi wa kimataifa nje ya lango kuu la uwanja huo.
Lango hilo hutumiwa na vikosi vya kijeshi vya kigeni, ambapo bado haijabainika endapo walinusurika na shambulio hilo.
Msemaji wa polisi alisema, shambulio hilo lilifanyika karibu na ofisi za safari za ndege nchini humo zilizoko nje ya uwanja.
Shambulizi hilo linafanyika ikiwa ni siku tatu baada ya mwanamgambo mmoja kuwaua watu 14 wakiwemo raia tisa wa kigeni mjini humo.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru