Sunday 17 May 2015

Rodgers:Hakuna kama Gerrard





KOCHA wa Mkuu wa Liverpool, Brendan Rodgers, amesema hakuna mchezaji anayeweza kuchukua nafasi ya nahodha Steven Gerrard.

Rodgers alisema kuondoka kwa Gerrard katika kikosi hicho ni pengo kubwa kwa kuwa nahodha huyo alikuwa hodari na mtu aliyejituma.

Kocha huyo alisema mchezaji huyo alikuwa ni moja ya wachezaji ambao wameisaidia Liverpool kupata mafanikio makubwa.

"Kuna wachezaji wengi na wazuri England, lakini  Liverpool haiwezi kupata mchezaji mzuri kama Gerrard ambaye hawezi kufananishwa na mchezaji yeyote kutokana na mchango wake," alisema Rodgers.

Nyota huyo aliagwa juzi katika mchezo wake wa mwisho ambapo Liverpool ilikubali kipigo cha mabao 3-1, katika mchezo uliopigwa katika dimba la Anfield.

Mchezaji huyo alijiunga na klabu hiyo miaka 17 iliyopita na msimu ujao atavaa jezi ya LA Galax





Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru