RAIS
Pierre Nkuruzinza, ametoa onyo kali kuhusiana na jaribio lingine lolote la
kutaka kuchukua madaraka ya nchi hiyo kwa kutumia nguvu.
Alisema
jaribio la namna hiyo halipaswi kufanyika tena na serikali itahakikisha
inakabiliana na makundi yenye nia ya kuvuruga amani kwa kuwa vitendo hivyo
vitasababisha umasikini na vita.
Nkuruzinza
alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku mbili baada ya Marekani kumuonya kutoendelea na
nia ya kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Marekani
imesema kitendo cha Nkuruzinza kugombea tena urais, kitazorotesha usalama
nchini humo na kutishia misaada ya kimataifa.
Msemaji
wa Ikulu ya Marekani, Jeff Rathke, alisema nchi hiyo inawasiwasi kufuatia
uwezekano wa kutokea ghasia zaidi baada ya Nkurunziza kurejea Burundi.
Alisema
Marekani inamtambua Nkurunzinza kama rais halali wa Burundi licha ya kusisitiza
kiongozi huyo kutowania muhula wa tatu.
Baadhi
ya maofisa wa kijeshi walioshiriki kuongoza mapinduzi wamekamatwa huku wengine
wakitokomea na kusakwa na majeshi watiifu wa serikali.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Generali
Godefroid Niyombare, anaendelea kusakwa
Sunday, 17 May 2015
Nkuruzinza aonya
08:36
No comments
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Toa Maoni Yako Kwa Uhuru