Sunday 17 May 2015

Nkuruzinza aonya





RAIS Pierre Nkuruzinza, ametoa onyo kali kuhusiana na jaribio lingine lolote la kutaka kuchukua madaraka ya nchi hiyo kwa kutumia nguvu.
Alisema jaribio la namna hiyo halipaswi kufanyika tena na serikali itahakikisha inakabiliana na makundi yenye nia ya kuvuruga amani kwa kuwa vitendo hivyo vitasababisha umasikini na vita.
Nkuruzinza alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku mbili baada ya Marekani kumuonya kutoendelea na nia ya kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Marekani imesema kitendo cha Nkuruzinza kugombea tena urais, kitazorotesha usalama nchini humo na kutishia misaada ya kimataifa.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jeff Rathke, alisema nchi hiyo inawasiwasi kufuatia uwezekano wa kutokea ghasia zaidi baada ya Nkurunziza kurejea Burundi.
Alisema Marekani inamtambua Nkurunzinza kama rais halali wa Burundi licha ya kusisitiza kiongozi huyo kutowania muhula wa tatu.
Baadhi ya maofisa wa kijeshi walioshiriki kuongoza mapinduzi wamekamatwa huku wengine wakitokomea na kusakwa na majeshi watiifu wa serikali.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Generali Godefroid Niyombare, anaendelea kusakwa

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru