Thursday 19 December 2013

JK kuchunguzwa afya


Na mwandishi wetu
RAIS Jakaya Kikwete ameondoka nchini juzi jioni kwenda Marekani kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Ikulu ilisema uchunguzi huo ni utaratibu wa kawaida.
Kwa mujibu wa ratiba ya shughuli za uchunguzi wa afya na umbali wa safari hadi Marekani na kurudi nchini, Rais Kikwete anatarajiwa kurejea Alhamisi ijayo.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru