Saturday 21 December 2013

Mawaziri kufumuliwa


WAANDISHI WETU, DAR NA DODOMA
BAADA ya mawaziri wane kuachia ngazi kutokana na kashfa ya Operesheni Tokomeza Ujangili, hofu ya kutemwa imetanda miongoni mwa mawaziri, imefahamika. Mawaziri waliojiuzulu baada ya shinikizo la wabunge kutaka wawajibike ni Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi), Shamsi.
Kujenga Taifa) na Dk. David Mathayo (Maendeleo ya Mifugo na
Uvuvi). Habari ambazo Mzalendo imezipata, zinaeleza kuwa
Rais Jakaya Kikwete anatarajia kufumua baraza la mawaziri, huku baadhi ya waliomo wakidaiwa kuachwa kutokana na utendaji na kuhusishwa na kashfa ya ujangili.
Kwa mujibu wa habari hizo, mabadiliko hayo huenda yakatangazwa wakati wowote kuanzia sasa na huenda yakawafanya baadhi ya mawaziri kusherehekea Krismasi na Mwaka Mpya kwa huzuni.
Chanzo cha habari kimebainisha kuwa baadhi ya mawaziri ambao wako katika hatari ya kuachwa wamekuwa katika
wakati mgumu baada ya ripoti ya Kamati ya Bunge ya Ardhi,
Maliasili na Mazingira kuwatuhumu kuwa wana uhusiano katika
ujangili ama kupitia ndugu zao au wanasiasa.
“Kwa jumla hali ni tete baada ya ripoti ya (James) Lembeli
(mwenyekiti wa kamati hiyo) kuwasilishwa na baadhi ya wabunge
na mawaziri kudaiwa kuhusika kwenye mtandao wa ujangili. Wengi wamejawa hofu huku baadhi wakisema wazi kwamba hawana hakika na hatima yao,” kilisema chanzo chetu.
Mbali na mawaziri waliojiuzulu kisha na Rais Kikwete kuridhia na kutengua uteuzi wao, pia wamo baadhi ya mawaziri ambao
wabunge wamekuwa wakitaka watimuliwe.
Licha ya ripoti ya Lembeli, wakati wa mjadala wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) iliyowasilishwa wiki
iliyopita, Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugora, alitamka
bayana kwamba Rais anapaswa kumtimua Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Nchi, Ofi si ya Waziri Mkuu (TAMISEMI),
Hawa Ghasia, kwa kushindwa kuchukua hatua dhidi ya watendaji
wanaofanya ubadhirifu wa malimioni ya shilingi. Mbunge huyo pia pamoja na wengine, juzi walisisitiza kuwa Waziri Mkuu anapaswa kuwajibika kwa kuwa kasoro zilizojitokeza kwenye operesheni tokomeza pamoja na ubadhirifu unaofanywa
na maofi sa wa serikali katika wizara mbalimbali.
Hilo pia liliwekewa msisitizo baada ya Moses Machali (Kasulu Mjini- NCCR Mageuzi) ambapo alisema wabunge wanatafuta saini kwa ajili ya kuwasilisha hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani
na Pinda.
Mbali na mawaziri hao, Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA), Mchungaji Peter Msigwa, alisema Waziri wa Nchi Ofi si ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika, pia anapaswa kuwajibika kwa kuwa maofi sa wa Usalama wa Taifa, walishiriki katika operesheni hiyo ambayo imelitia doa taifa.
Hofu ya kupanguliwa kwa baraza la mawaziri pia inakuja baada ya hivi karibuni kuwepo kwa orodha ya mawaziri ambao wamekuwa wakidaiwa kikwazo katika utekelezaji wa majukumu
yao. `
Mawaziri hao ni Christopher Chiza (Kilimo, Chakula na Ushirika) na naibu wake Adam Malima, Dk. William Mgimwa (Fedha), Dk. Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi) na Dk. Abdallah Kigoda (Viwanda na Biashara).
Dalili za kuwepo kwa mabadiliko ya baraza hilo zilianza kuonekana kabla ya kuanza kwa mkutano wa bunge uliomalizika
jana, baada ya Rais Kikwete kumteua Dk. Asha Rose Migiro kuwa mbunge.
Wakati huo huo, serikali imewapongeza mawaziri wane waliojiuzuru jana kwa hiari yao ili kulinda heshima na imani ya
wananchi kwa serikali yao.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuwa akihitimisha bunge mjini hapa. Pinda alisema serikali
imesikia uamuzi huo wa mawaziri mawaziri wa kuona ni vyema
wakajiudhuru.
Alisema serikali inawapongeza mawaziri hao kwa kuonyesha ujasiri
wao kwa kutambua dhamana yao na Rais Jakaya Kikwete ameridhia.
Pinda alisema serikali itaendelea kuyafanyia kazi mapendekezo ya
kamati ya Bunge kuhusiana na Operesheni tokomeza iliyotolewa juzi iliyosababisha mawaziri hao kujiudhuru.
Alisema katika taarifa hiyo ya kamati matatizo mbalimbali yalijitokeza ikiwemo mateso dhidi ya watuhumiwa, matumizi mabaya ya silaha, uchomaji wa nyumba za wananchi na kuua mifugo.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru