Tuesday 15 October 2013

DC aumizwa shule kukosa madawati


Na Theodos Mgomba, Dodoma
SHULE za sekondari za kata na zile za msingi wilayani Bahi, zinakabiliwa na upungufu mkubwa wa madawati na maabara.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Betty Mkwasa alisema hayo alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari waliotembelea wilaya hiyo hivi karibuni.
Betty alisema licha ya wilaya hiyo kuwa na vitabu vya kutosha, upungufu huo wa madawati kwa shule za msingi na maabara kwa shule za sekondari ni tatizo kubwa.
Alisema katika shule 20 za sekondari zilizopo wilayani humo, ni shule nane tu ndizo zenye maabara, na kwamba zimekuwa zikifanya kazi.
Alisema hali hiyo imekuwa ikiwavunja moyo wanafunzi ambao wanapenda kusoma masomo ya sayannsi kwani hawama maabara.
Hata hivyo, mkuu huyo alisema kwa upande wa madawati, shule zilizoathirika zaidi na upungufu huo ni zile za msingi.
“Suala la madawati kwa shule zetu za msingi bado ni tatizo, kwani katika shule nyingi za msingi bado kuna idadi kubwa ya wanafunzi ambao wanakaa chini,” alisema Betty.
Mkuu huyo wa wilaya alisema wilaya yake inaendelea na mikakati mbalimbali ya kutatua tatizo hilo la madawati kwa shule za msingi.
Alisema moja ya mikakati ya kuondokana na tatizo hilo ni kuingiza suala la madawati na maabara katika bajeti ya halmashauri ya mwaka huu.
Mkuu huyo alisema kwa kupitia bajeti hiyo, ana uhaki


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru