Wednesday 30 October 2013

January awapigia debe walima chai


Na mwandishi wetu, Bumbuli
NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, ametoa wito kwa viwanda vya chai vya Herkulu na Dindira kuongeza uzalishaji.
Lengo ni kutaka wanunue zao hilo kwa wingi toka kwa wakulima wa chai wa Bumbuli, ambao awali walikuwa wakihudumiwa na Kiwanda cha Mponde.
Kiwanda cha chai cha Mponde kimefungwa kufuatia mgogoro baina ya wakulima wa chai na Chama cha Wakulima wa Chai cha Usambara (UTEGA) na mwekezaji.
January, ambaye pia Mbunge wa Bumbuli alikuwa akizungumza na wakulima katika Kijiji cha Tamota hivi karibuni.
Alisema hivi sasa majani ya chai ni mengi, hivyo hatua ya viwanda hivyo kuongeza uzalishaji itawapatia unafuu wakulima.
Hata hivyo, alisema amekwisha zungumza na uongozi wa viwanda hivyo, ili viongeze uzalishaji na vifaa vya kusafirishia chai hiyo kutoka shambani hadi kwenye viwanda.
January, alitoa wito pia kwa wakulima, kuwa wavumilivu wakati huu ambapo kuna mpango wa kuweka menejimenti ya muda kama ilivyokubaliwa na serikali, ili kiwanda
hicho kianze kazi ya usindikaji.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru