Thursday 13 November 2014

Ajinyonga kisa? Wivu wa mapenzi


NA CHIBURA MAKORONGO,KAHAMA 

MFANYAKAZI wa kampuni ya uchambuaji pamba ya Kahama Oil Mills Ltd, Yusuph Abdallah (55) amekutwa amekufa bafuni baada ya kujinyonga kutokana na wivu wa mapenzi. 
Mwenyekiti wa Mtaa wa Mhongolo, Elias Chuma,  alisema tukio hilo lilitokea juzi  saa tano asubuhi, baada ya mfanyakazi wa usafi wa nyumba ya kampuni aliyokuwa anakaa Abdallah, Pili Makoye, kumkuta Abdallah akiwa amejinyonga.  
Kiongozi huyo alisema baada ya kuona hivyo, Pili alipiga owe ambapo watu walifurika na kushuhudia tukio hilo. 
Mwenyekiti huyo alisema kuna taarifa kwamba Abdallah alikuwa mgogoro wa muda mrefu wa kifamilia hali iliyomfanya atoweke  nyumbani kwa muda mrefu huku akimtamkia mkewe kwa maneno makali. 
Chuma aliwaeleza waandishi wa habari kwamba  kabla ya kujinyonga, Abdallah alimuwekea mtoto wake sh. 38,500 mfukoni ili zimsaidie.Alisema walikuwa na mgogoro wa kifamilia wa muda mrefu ambapo ulianza  Ijumaa iliyopita, hivyo kuamua kuondoka nyumbani kwa siku kadhaa. 
Aliporejea nyumbani, mkewe naye aliamua kuondoka na ndipo
mwanamume huyo alipochukua jukumu la kujinyonga. 
Kwa mujibu wa Chuma, siku ya tukio Abdallah alirudi nyumbani kwake na mkewe, na kuaga kuwa anakwenda kwa dada yake kuishi huku akimtelekeza mtoto wa miaka mitano ambaye wakati anakwenda kujinyonga alimwachia fedha hizo na kuaga anakwenda kujisaidia.  
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Justus  Kamugisha,  alithibitisha tukio hilo na kueleza kwamba lilitokea juzi.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru