Thursday 13 November 2014

Mauaji ya Kiteto yalitikisa Bunge


JESHI Polisi linawashikilia watu watano kuhusiana na mauaji katika mapigano kati ya wafugaji na wakulima katika kijiji cha Matui wilayani Kiteto.
Katika mapigano hayo, watu wanne waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Akitoa kauli ya serikali bungeni jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mathias Chikawe, alisema mapigano hayo yalitokea juzi katika wilaya hiyo.
Chikawe alisema Jumanne iliyopita katika kijiji hicho, mkulima Hassan Kondeja, mkazi wa Kijiji cha Bwawani, alikwenda katika Kituo cha Polisi Matui kutoa malalamiko kuwa kuna wafugaji wameingiza mifugo yao katika shamba lake la mihogo.
Waziri huyo alisema mkulima huyo aliwaambia polisi kuwa, anawafahamu wafugaji hao na atakwenda nyumbani kwao kuzungumza nao ili kumaliza tatizo hilo.
Alisema utaratibu huo wa kuzungumza uliwekwa na wanakijiji wenyewe ili kuondoa migogoro.
ìPolisi baada ya kuambiwa hivyo, walikubaliana na mlalamikaji huyo na kumruhusu kwenda kuzungumza na wafugaji hao,íí alisema.
Waziri Chikawe alisema juzi mkulima huyo alikutwa ameuawa na kuzikwa katika shamba lake huku kichwa kikiwa nje.
Alisema baada ya wanakijiji wenzake kupata taarifa hiyo na hasa wale wa kabila lake, walijikusanya na kuanza kuchoma moto maboma ya wamasai na kuswaga mifugo yao.
Kwa mujibu wa Chikawe, katika muendelezo wa kuswaga mifugo hiyo, wakulima hao walikutana na mama mmoja wa kimasai akiwa amebeba mtoto wa miaka minne mgongoni.
Waziri huyo alisema wakulima hao walimkatakata mama huyo na kumuua huku wakimuacha mtoto huyo bila kumdhuru.
Chikawe alisema mpaka sasa, mbali ya kuwakamata watuhumiwa hao watano, pia wamekamata ngíombe 309 walioibwa katika mapigano hayo.
Alisema ngíombe hao walikamatwa katika eneo la Kijiji cha Chitego, wilayani Kongwa na wengine katika eneo Chemba.
Hata hivyo, Chikawe alisema hali katika eneo hilo bado haijarudi kuwa nzuri, licha ya viongozi wa serikali wa mkoa kwenda katika eneo la tukio.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru