Thursday 13 November 2014

Mgimwa awapa darasa waongoza watalii


NA JAMES LANKA, MOSHI
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utaliii, Mahmoud Mgimwa, amewataka waongoza watalii kuhakikisha wanapewa  mikataba halali ya kazi na wamiliki wa kampuni wanayofanyakazi ili kuepuka kunyonywa haki zao. 
Mgimwa alitoa rai katika mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Waongoza Watalii Mlima Kilimanjaro (KGA), kilichofanyika juzi mjini hapa.
Mwenyekiti wa chama hicho, Respicius Baitwa, alimueleza naibu waziri kuwa,  pamoja na ugumu wa kazi yao, baadhi ya wamiliki wa kampuni za utalii wamekuwa wakiwanyonya haki zao waongozaji hao.
 “Nimesikiliza risala yenu kwa makini, changamoto kubwa mliyoeleza ni maslahi duni kutokana na kulipwa ujira mdogo na waajiri wenu, hivyo nawasihi muwe makini, hasa katika suala la mikataba yenu ya kazi ili serikali iweze kutetea haki zenu, maana ninyi ni mabalozi wa utalii,” alisema.
Waziri huyo aliwaahidi waongoza watalii hao kuwa atakutana na Chama cha Wamiliki wa Kampuni ya Utalii nchini (TATO), pamoja na Chama  cha Wamiliki wa Kampuni ya Utalii Kilimanjaro (KIATO), ili kuona namna ya kulinda maslahi ya waongoza watalii hao.
Mgimwa alisema Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, ambayo inaiingizia serikali mapato makubwa, inapaswa kuwa na wafanyakazi makini na wanaofanya kazi zao kwa uadilifu. 

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru