Thursday 13 November 2014

JK azungumza na viongozi



NA MWANDISHI WETU
Rais Dk. Jakaya Kikwete akiwa hospitalini nchini Marekani
Taarifa ya Ikulu ilisema jana kuwa Rais Kikwete ameanza kuwasiliana na mamia kwa mamia ya wananchi nchini na kujibu ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) wa kumpa pole na kumtakia heri.
Tangu alipofanyiwa upasuaji wa tezi dume wiki iliyopita, Rais Kikwete amepokea mamia kwa mamia ya SMS zikimpa pole na kumtakia nafuu ya haraka.

“Rais Kikwete bado anaendelea kujibu SMS hizo na wananchi ambao wamemtumia, waendelee kusubiri majibu yake kwa sababu anakusudia kujibu SMS zote ambazo ametumiwa,” ilisema taarifa hiyo.

Aidha, Rais Kikwete jana alizungumza kwa simu na uongozi wa juu kwa mara ya kwanza tangu afanyiwe upasuaji. Rais alizungumza na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru