Tuesday 25 June 2013

Brandts akuna kichwa


NA MWANDISHI WETU
KOCHA mkuu wa Yanga Eenest Brandts, amesema anatarajia kuanza maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara itakayoanza kutimua vumbi Agosti mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Brandts alisema mapambano kwa ajili ya msimu huo yatafanyika ili Yanga itetee ubingwa wa Tanzania bara iliyoutwaa msimu uliopita.
Brandts alisema, ratiba ya maandalizi kwa timu yake, itaanza rasmi mwanzoni mwa wiki ijayo kwa mazoezi mepesi kabla ya kuanza kambi.
Alisema, wachezaji wake walipewa mapumziko ya wiki mbili, anaamini wamepumzika vya kutosha hivyo kazi iliyopo mbele yao ni kuanza maandalizi kwa ajili ya msimu ujao.
Alisema wakati kikosi chake kikifanya mazoezi hayo, maandalizi kwa ajili ya kambi ya kudumu kabla ya kuanza kwa ligi hiyo, yanaendelea na anataka kuona timu inakuwa kambini muda mrefu.
Brandts alisema, anataka wachezaji wake wazoeane ndiyo maana anataka wawe kambini kwa muda mrefu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru