Thursday 20 June 2013

Mbowe, Lema wajisalimisha Polisi Arusha


MWENYEKITI wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wamejisalimisha kwa jeshi la polisi leo asubuhi. Wanasiasa hao walipewa onyo la kujisalimisha jana kwa ajili ya kutoa ushahidi kuhusu madai yao kuwa wanawafahamu polisi waliolipua bomu kwenye mkutano wa hadhara.
Hata hivyo, habari kutoka ndani ya jeshi hilo zinasema kuwa, Mbowe amekanusha kusema kuwa ana ushahidi kuhusu polisi waliolipua bomu hilo wakati akihojiwa na maofisa wa polisi. Lakini baadaye baada ya kuachiwa kwa dhamana na kuzungumza na waandishi wa habari, alidai tena ana ushahidi na atauwasilisha kwenye tume maalumu itakayoundwa kuchunguza tukio hilo.
Habari zaidi, soma gazeti la Uhuru kesho Ijumaa.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru