Tuesday 25 June 2013

Taasisi za Tanzania zabeba tuzo tatu Ghana


NA MWANDISHI WETU
TANZANIA imeshinda tuzo tatu za juu za ubunifu katika Utumishi wa Umma, barani Afrika, kufuatia taasisi zake tatu kushinda nafasi ya kwanza na kunyakua vikombe vya ushindi.
Vikombe hivyo vimekabidhiwa na Rais wa Ghana, John Mahama wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma Afrika, yaliyofanyika mjini Accra.
Taasisi za Tanzania zilizoshinda ni Ofisi ya  Ukaguzi ya Taifa, (NAO), Wakala wa Vipimo, (WMA) na Wakala wa Vitambulisho vya Taifa, (NIDA), ambapo zilifanya vizuri kwenye maonyesho ya  siku 7 ya shughuli za utumishi wa umma yaliyofikia kilele mwishoni mwa wiki.
Akizungumzia ushindi huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani, alisema Tanzania ilistahili ushindi kutokana na taasisi zilizoshiriki kufanya kazi zake kwa ufanisi.
Pia, alisema amefarijika kwa taasisi hizo kupata ushindi mkubwa katika maonyesho hayo, ambapo taasisi 42 kutoka Tanzania zilishiri.
Katika hotuba yake Celina, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mawaziri wa Utumishi Afrika, aliwataka watumishi wa umma kuwatumikia wananchi kwa bidii, unyenyekevu, uadilifu na kueleza utumishi wa umma ni kuwatumikia watu.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi, amekiri kuwa Tanzania ni moja ya nchi zinazofanya vizuri katika maonyesho hayo Afrika

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru