Tuesday 25 June 2013

Rooney atakiwa Barcelona


MADRID, Hispania
BARCELONA nayo imeingia vitani kuwania saini ya mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney.
Mbali ya Barcelona, Chelsea na Real Madrid zimeonyesha nia ya kumtaka nyota huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya England.
Barcelona iko tayari kutoa pauni milioni 25 (sawa na sh. Bilioni 62.5) kuwezesha Rooney kutua Nou Camp.
Rooney (27), wiki hii alitarajiwa kufanya mazungumzo na kocha wake David Moyes kuhusu mustakabali wake ndani ya Old Trafford.
Kabla ya kustaafu, Sir Alex Ferguson alisema, Rooney hatauzwa baada ya mshambuliaji huyo kuomba kuondoka Man United.
Vyanzo vya uhakika ndani ya Barcelona vinaeleza kuwa, klabu hiyo inafuatilia mchakato mzima kuhusu nafasi ya Rooney na kama Man United itaamua kumpiga bei, itakuwa tayari kumnyakua.
Mtoa habari mmojawapo alisema: “Rooney ni mshambuliaji ambaye atamudu mfumo unaotumiwa na Barcelona.
“Kwa Barcelona, ulinzi unaanza kuanzia mbele na Rooney anafanya kazi ukilinganisha na wengine.
"Ni mchezaji mzuri ana vigezo vyote. Klabu yake ikimuweka sokoni, Barcelona iko tayari kuwania saini yake.”

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru