Tuesday 20 August 2013

Exim yaadhimisha miaka 16 ya huduma



Mwandishi Wetu
BENKI ya Exim Tanzania imetimiza miaka 16 katika utoaji  huduma za kibenki, ikijivunia mkakati utakaoifanya kuwa bora zaidi nchini katika miaka michache ijayo.
Ilianza kutoa huduma za kibenki nchini Agosti 15, 1997, kwa kuwa na tawi moja jijini Dar es Salaam, ambapo sasa inayo 25 nchini
.
Akizungumza katika maadhimisho yaliyofanyika makao makuu ya benki hiyo, jijini Dar es Salaam, Ofisa Mtendaji Mkuu, Dinesh Arora, alisema imejikita katika utoaji huduma za kibenki za kipekee.
Kwa mujibu wa Arora, benki hiyo imeorodheshwa kwenye tunzo za benki bora Afrika, zilizofanyika jijini Marrakesh, Morocco.
“Tutaendelea na jitihada za kutoa huduma. Mafanikio haya katika kipindi hiki yametokana na dhamira yetu ya kutoa huduma za kibenki za kipekee, zitokanazo na wafanyakazi makini na wateja waaminifu,’’ alisema.
Ofisa huyo alisema benki hiyo inaamini ugunduzi ni maisha, hivyo wateja watarajie huduma bora.
Naye Meneja wa Huduma kwa Wateja, Frank Matoro, alisema  maadhimisho hayo yatakuwa chachu ya kuendelea kutoa huduma bora, kwa kuwa kipaumbele cha Exim ni utoaji huduma bora kwa wateja.
Alisema hilo ndilo limeifanya benki kuanzisha huduma ya mawasiliano kwa wateja kupitia mtandao.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru