Wednesday 21 August 2013

Kero za muungano zaanza kutatuliwa


NA MWANDISHI WETU
KAMATI ya pamoja ya kushughulikia kero za muungano, imefanikiwa kuzipatia ufumbuzi baadhi.
Moja kati ya hoja hizo ni Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu kutofanya kazi Zanzibar kutokana na sheria hiyo kutokuwa suala la Muungano.
Msemaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais Siglinda Chipungaupi, alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jana, kuhusu mafanikio ya ofisi hiyo.
Siglinda, alisema sheria hiyo imefanyiwa marekebisho kupitia Sheria ya Marekebisho ya sheria mbalimbali ikiwemo namba 8 ya 2006 na kuondoa upungufu uliokuwepo na sasa inafanya kazi pande zote mbili.
Alisema hoja nyingine ni ushiriki wa Zanzibar katika Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC), ambapo nafasi ya Zanzibar kuwasilisha miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa ajili ya kuijumuisha katika miradi ya kikanda ya EAC.
Kwa mujibu wa msemaji huyo, SMZ iliwasilisha miradi tisa katika miradi ya Tanzania itakayoombewa ufadhili chini ya EAC.
Alisema Wizara ya Afrika Mashariki inaendelea kufuatilia miradi hiyo kwa kushirikiana na sekta husika.
Hoja nyingine iliyopatiwa ufumbuzi ni ya mgawanyo wa mapato yatokanayo na misaada kutoka nje.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru