Wednesday 16 April 2014

Dk. Magufuli, we acha tu


NA WILLIAM SHECHAMBO
MKUTANO wa Baraza la Wafanyakazi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), uliopangwa kufanyika jana, mkoani Tanga, umesitishwa kwa agizo la  Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli.


Inadaiwa kuwa kafanya hivyo ili kutoa fursa kwa wahandisi kuongeza nguvu kwenye ukarabati wa miundombinu iliyoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.
Agizo hilo lilisababisha ratiba ya taasisi hiyo ya serikali ya kuendelea na mkutano mkoani Tanga kupigwa kalenda.
Akizungumzia hatua hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Alhaj Mussa Iyombe, alisema mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu nchini, hali inayowalazimu watendaji kufanya kazi kadri inavyowezekana ili kurudisha huduma katika hali ya kawaida.
Awali, Waziri Magufuli alipokuwa akikagua uharibifu uliotokea katika daraja la Mpiji Bagamoyo, mkoani Pwani, alisema TANROADS wanatakiwa kuhakikisha wanafanyakazi mchana na usiku ili barabara hiyo muhimu na yenye kupitisha magari mengi ifunguliwe haraka iwezekanavyo.
Dk. Magufuli, alisema shughuli za uchimbaji wa mchanga zinazofanywa karibu au chini ya madaraja na maeneo ya karibu na barabara, ndicho chanzo cha mito kuhama kutoka katika njia yake ya asili na kuharibu miundombinu ya barabara.
Aliwatahadharisha wananchi kuepuka tabia hiyo.
Mvua kubwa zilizonyesha katika maeneo mbali mbali nchini toka wiki iliyopita, zimesababisha madhara makubwa kwa upande wa miundombinu ya barabara kwa kusomba madaraja na kuvunja kingo za mitaro.
TANROADS kwa kushirikiana na kampuni za ujenzi za SKOL na Estim Construction Company Ltd zote za Dar es Salaam, tayari wameanza kazi za kurekebisha sehemu kadhaa ikiwemo daraja la Mpiji

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru