Friday 11 April 2014

Mbio za Mwenge kuzinduliwa Kagera


NA KHADIJA MUSSA

MKOA wa Kagera unatarajia kuzindua miradi ya maendeleo yenye thamani ya sh. bilioni 14 katika hafla ya uzinduzi wa mbio za mwenge, itakayofanyika Mei 2, mwaka huu.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, ambapo wananchi zaidi ya 30, 000 wanatarajiwa kuhudhuria, wakiwemo viongozi wa ndani na nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa mkoa huo, Kanali Mstaafu Fabian Massawe alisema miradi ikayozinduliwa ni ya sekta za afya, elimu na uchumi.

Alisema baada ya kuzinduliwa kwa mwenge huo, utakimbizwa katika halmashauri nane za mkoa huo, ambako utazindulia miradi hiyo ya maendeleo.

Massawe alitumia fursa hiyo kuwaomba wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, kujitokeza kwenda kuwekeza katika mkoa huo, ambao una fursa nyingi.

Alisema kauli mbiu ya mbio hizo kwa mwaka huu ni 'Katiba ni sheria kuu ya nchi, watanzania wajitokeze kupiga kura ili wapate katiba bora.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru