Friday 11 April 2014

Mvua kuongezeka nchini- TMA


NA MWANDISHI WETU

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini (TMA), imetoa tahadhari ya uwepo wa mvua kubwa inayozidi milimita 50 kuanzia leo hadi Jumatatu.

Kufuatia kuwepo kwa mvua hiyo, mamlaka imewataka wakazi wa maeneo hatarishi, watumiaji wa bahari pamoja na mamlaka zinazohusika na maafa, kuchukua tahadhari stahiki.

Mikoa inayotarajiwa kupata mvua hiyo ni ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Visiwa vya  Unguja na Pemba na uwezekano wa kusambaa katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Morogoro.

“Hali hii inatokana na kuimarika zaidi kwa ukanda wa mvua 'Inter-tropical convergence zone (ITCZ)', ambao umeambatana na ongezeko la unyevunyevu katika eneo la bahari ya Hindi,” ilisema taarifa hiyo.

Mvua hiyo inatarajiwa kuambatana na upepo mkali unaozidi kilometa 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita mbili katika ukanda wa pwani.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru