Monday 27 October 2014

Dk Bilal mgeni rasmi tamasha la MOWE leo


NA EMMANUEL MOHAMED
MAKAMU wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tamasha la wanawake wajasiriamali mali (MOWE), litakalofanyika leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es salaam.  


Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa tamasha hilo, Helihaka Mrema, alisema tamasha hilo lina lengo la kuwakutanisha wajasiriamali hao na wadau mbalimbali ili kuboresha ubora wa bidhaa zao kwa lengo la kukidhi haja ya masoko ya ndani na nje.
Helihaka alisema tamasha hilo litawakutanisha wajasiriamali zaidi ya 158 na wadau mbalimbali, ikiwemo Wakala wa Vipimo Tanzania, Benki ya Wanawake (TWB), Shirika la Viwanda Vidogovidogo (SIDO) na Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA).
Alisema wadau hao watasaidia kutoa elimu ili bidhaa zao ziweze kukidhi haja katika masoko yao, hususan wanaozalisha bidhaa za chakula, dawa na nguo.
"Changamoto ya masoko kwa wajasiriamali ni suala la muda mrefu na ufumbuzi wake ni elimu kutoka kwa wadau, wakiwemo wakala wa vipimo na TFDA ili bidhaa zetu ziweze kukidhi soko," alisema.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru