Monday 27 October 2014

Machangudoa Moro wanyooshewa kidole


NA LATIFA GANZEL, MOROGORO
HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro, imewataka wanawake wanaojihusisha na biashara ya ngono katika eneo la Msamvu  maarufu Itigi, kuacha mara moja.
Imeonya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakaokaidi amri hiyo kwa kuwa ni kinyume cha sheria.
Agizo hilo lilitolewa juzi na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amiri Nondo, ambapo alisema biashara hiyo ni haramu na kamwe haitaachwa iendelee.
“Nilifanya ziara ya kushitukiza katika eneo la Itigi Msamvu.  Eneo  lile limechafuliwa sana na wanawake hao wanaofanya biashara za kuuza miili.  Kuna  magari makubwa yanasimama hapo ndiyo sababu ya kuwepo kwa baishara hiyo,’’ alisema.
Alisema  halmashauri hiyo imebaini kuwepo kwa matumizi mabaya ya vibanda vya mawakala wa simu za mkononi, ambavyo hutumika kama vyumba vya kufanyia bishara hiyo haramu.
“Tumeagiza wenye vibanda vilivyojengwa bila utaratibu kubomoa kabla ya halamshauri kuchukua hatua ya kuwabomolea. Wakisubiri tufanye hivyo itawagharimu,’’ alisema meya huyo.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru