Wednesday 12 February 2014

Mzimu wa Zitto watikisa

NA PETER KATULANDA, MWANZA

WAKATI mzimu wa Zitto Kabwe ukizidi kukimomonyoa

Zitto Kabwe Mb. (CHADEMA)
CHADEMA katika maeneo mbalimbali nchini, hususan mkoani Mwanza, Chama  Cha Mapinduzi (CCM) mkoani humo kinazidi kujiimarisha kwa kuzoa wanachama wapya.
Katibu Mwenezi wa CCM mkoani Mwanza, Simon Mangelepa, aliiambia Uhuru jana kuwa, kwa kipindi cha wiki moja Chama
kimepata wanachama wapya 1,596 wakiwemo 1,206 kutoka CHADEMA.
Alisema, wamepata wanachama hao wakati wa wiki ya
maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa kwa CCM, katika wilaya mbalimbali  za mkoa huo na kutamba kwamba, CHADEMA wajiandae kung’oka katika majimbo yote waliyoshinda katika uchaguzi Mkuu uliopita mkoani humo.
“Nawapongeza wanachama wapya waliojiunga na Chama Bora wakati wa maadhimisho ya miaka 37, watambue wajibu wa kiapo walichokula wakati wakikabidhiwa kadi za CCM na kudumisha amani na mshikamano na watanzania wote, CCM hatuna sera ya ‘kukunja ngumi’,” alisema Mangelepa.
Katibu huyo alifafanua wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika Januari 26 hadi Februari 5, mwaka huu, katika kila wilaya, CCM ilivuna wanachama 1,596 wakiwemo 180 waliojiunga na jumuia zake.
Alizitaja jumuia hizo na wanachama wake wapya kwenye mabano kuwa ni UVCCM (80), UWT (50) na Wazazi (50) katika wilaya zote za mkoa huo.
Alisema wananchi 1,416 walijiunga na Chama katika wilaya tano za Sengerema (39), Kwimba (67), Misungwi (561), Nyamagana (520) na Ukerewe wanachama 229 na hivyo jumla kuwa 1,596.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru