Tuesday 18 February 2014

UWT yampongeza JK


Na Mwandishi Wetu


UMOJA wa Wanawake wa Tanzania (UWT) umempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa uteuzi wake wa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba lililoanza jana mjini Dodoma.
UWT imewataka wajumbe waliochaguliwa kuwepo katika bunge hilo kutambua dhamana waliopewa na Rais kwa kuhakikisha wanahakikisha wanawatetea wananchi ndani ya bunge hilo katika kupata Katiba Mpya.
Taarifa iliyotolewa jana na Naibu Katibu Mkuu (Bara) wa UWT, Eva Kihwele, ilisema wajumbe wanapaswa kuzingatia ueledi na uadilifu katika kutengeneza katiba ya Tanzania yenye kulinda kutetea na kusimamia maslahi ya taifa.
"Katibu Mkuu wa UWT, Amina Makilagi, anampongeza Rais Kikwete kwa uteuzi huo, kwa kuwa umezingatia uwakilishi wa makundi mbalimbali ya kijamii na hasa kutimiza 50/50 ya uwakilishi wa wajumbe,''alisema.
Hivyo, UWT ilisema inawatakia kazi njema katika kuhakikisha wanalijenga taifa moja na imara katika upatikanaji wa Katiba mpya.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru