CHAMA cha Waandishi wa Habari
Wanawake Tanzania (TAMWA),
leo wanatarajia kuzindua ripoti ya utafiti wa kijinsia uliofanyika Desemba,
mwaka jana katika wilaya 20 za Tanzania.
Ripoti hiyo inatarajiwa kuzinduliwa
katika ofisi za TAMWA zilizoko Sinza Mori, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA,
Valerie Msoka, alisema jana kuwa uzinduzi huo unatokana na utafiti uliofanyika
baada ya mafunzo kutolewa kwa waandishi wa habari juu ya
habari za uchunguzi kuhusu a ukatili wa kijinsia, chini ya ufadhili wa Shirika
la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu UNFPA.
Alisema ripoti hiyo ya utafiti
inaonyesha hali halisi ya unyanyasaji wa kijinsia katika jamii pamoja na mambo
yanayokwamisha juhudi za vyombo vinavyotetea haki za wanawake na watoto hapa
nchini.
Kwa mujibu wa Valerie, utafiti huo ulifanywa
kwa kushirikiana na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali.
Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema
waandishi wa habari waliweza kuwahoji wanajamii mbalimbali kuanzia ngazi za
familia na kupata ukweli wa hali halisi ya unyanyasaji wa kijinsia ikiwemo,
ukeketaji, ubakaji, mauaji ya vikongwe, mimba katika umri mdogo na watoto wa
kike kulazimishwa kuolewa.
Wilaya ziliyofanyiwa utafiti ni
Kahama (Shinyanga), Tarime (Mara), Sengerema (Mwanza), Newala (Mtwara), Mbulu
(Manyara), Singida Vijijini (Singida), Bariadi (Simiyu), Busega (Simiyu), Nkasi
(Rukwa), Dodoma (Dodoma), Babati (Manyara), Chunya (Mbeya) na Bunda (Mara).
Kwa upande wa Zanzibar utafiti ulifanywa katika wilaya sita
za mikoa ya Mjini Magharibi, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Unguja Kusini na
Kaskazini Unguja.
Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Toa Maoni Yako Kwa Uhuru