Wednesday 12 February 2014

Waliokodiwa na CHADEMA kufanya fujo watekelezwa

NA PETER KATULANDA, MWANZA

ZAIDI ya vijana 50 waliokodiwa na kupelekwa na CHADEMA katika Kata ya Nyasula wilayani Bunda, kwa lengo la kufanya vurugu na kuzuia wananchi kupiga kura kwa madai ya kulinda kura, wametelekezwa.

Joyce Masunga, Katibu wa CCM (M) Mwanza
Hata hivyo, vijana 10 wamefanikiwa kurejea jijini Mwanza na kuwashushia tuhuma nzito viongozi wa M4C Kanda ya Ziwa kwa kushindwa kutimiza makubaliano na badala yake kuwatekeleza.
Tayari baadhi wamejisalimisha kwa uongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza kufichua siri hizo na kuomba kujiunga na Chama.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Joyce Masunga, alisema kilichowapata CHADEMA ni fundisho kwa vyama vinavyoeneza vurugu na uchochezi badala ya kueleza sera za kuwakomboa watanzania.
Habari za kuaminika na kuthibitishwa na baadhi ya vijana waliokuwa kwenye msafara huo, zimesema wenzao zaidi ya 30 wamekwama mjini Bunda kutokana na kukosa nauli ya kurejea Mwanza.
“Wenzetu wamekwama Bunda kutokana na kuishiwa fedha, tunafanya utaratibu wa kuchangishana tuwatumie hata kwa M-Pesa warudi, hali ya Bunda ni mbaya na tulitaitiwa…” alisema kijana mmoja bila kufafanua jinsi walivyobanwa.
Baadhi ya wafuasi wa CHADEMA, wakionekana kushangazwa na kusononeshwa na matokeo hayo, juzi na jana asubuhi kwenye kijiwe maarufu cha Kemondo katika Kata ya Nyamagana, walisema viongozi wao waliwatelekeza bila kuwaaga baada ya matokeo kutangazwa.
Katibu wa M4C Kanda ya Ziwa, Tungaraza Njugu, na viongozi wenzake hawakuweza kupatikana kutokana simu zao kuzimwa.
“Niliwambia CHADEMA inatapatapa na inajua ‘itanyolewa’ na CCM ndiyo maana ilipeleka vijana wakafanye fujo na kuzuia wana CCM wasipige kura, cha moto wamekiona, wamevuna uasi waliokuwa wakipanda kwa kucharanga watu mapanga,” alieleza Masunga na kuwapongeza wananchi wote na wana CCM kwa ushindi walioupata.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru