Monday 10 February 2014

Vigogo wa TBA wachungulia jela.

NA FURAHA OMARY

ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Makumba Kimweri na mwenzake, wamehukumiwa kifungo cha miaka tisa jela au kulipa faini ya sh. milioni 15, kila mmoja.
Washitakiwa hao wametiwa hatiani kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na kutoa kibali cha ujenzi wa ghorofa 18 mtaa wa Chimara, Dar es Salaam, jirani na Ikulu.
Kimweri (60) na aliyekuwa Msanifu Mkuu wa TBA, Richard Maliyaga (55), waliohukumiwa adhabu hiyo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, walinusurika kwenda jela baada ya kulipa faini.
Hukumu ilisomwa na aliyekuwa Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Sundi Fimbo, aliyesikiliza shauri hilo. Kwa sasa amehamishwa katika mahakama hiyo.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru