Monday 10 February 2014

Hakuna Mtanzania aliyenyongwa China.

Na Mwandishi Wetu

WIZARA ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imekanusha taarifa zilizosamba kwenye mitandao ya kijamii kuwa kuna Watanzania 160 wamenyongwa nchini China kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya.
Imesema hakuna Mtanzania yeyote aliyenyongwa kama inavyodaiwa kwenye mitandao na vyombo vya habari.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Dar es Salaam kwa vyombo vya habari na wizara hiyo ilisema taarifa hizo ni za uvumi na hazina ukweli wowote.
Taarifa hiyo ilisema mtuhumiwa anmayedaiwa kunyongwa aliyefahamika kwa jina la Mapusa yupo hai, gerezani anatumikia kifungo cha maisha kwa kosa la kuingiza dawa za kulevya nchini humo.
Ilisema hivi karibuni mfungwa huyo alishiriki kuandaa maonyesho ya utamaduni wa Kiafrika wakati wa kuadhimisha sherehe za mwaka mpya wa China.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru