Friday 19 July 2013

Jecha Mwenyekiti mpya SUZA


Na mwandishi wetu
RAIS wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Sheni, amemteua Said Bakari Jecha, kuwa Mwenyeki wa Baraza la Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA).
Dk. Sheni alifanya uteuzi huo kwa mujibu wa madaraka aliyopewa chini ya kifungu Namba 9(1) cha Sheria ya Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Namba 8 ya 1999.
Pia, Dk. Sheni amemteua Abdulrahman Rashid kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB).
Dk. Sheni alifanya uteuzi huo kwa mujibu  wa uwezo aliopewa chini ya kifungu Namba  8 (a) (1) cha sheria ya Bodi ya Mapato Zaznzibar (ZRB) Namba 7 ya 1996 kama ilivyorekebishwa na Sheria Namba 8 ya 2009.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni Katibu Mkuu Kiongozi  Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, uteuzi wa Jecha unaanza leo na uteuzi wa Abdulrahman ulianza juzi.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru