Friday 12 July 2013

Tenga: Aluta kontinua


NA MWANDISHI WETU
RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametaka wachezaji wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ kushinda mchezo wa leo dhidi ya Uganda.
Tenga, amewataka wachezaji kujiamini na wasikaribishe makosa ambayo yatatoa fursa kwa Waganda kupata bao.
Kingozi huyo alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na wachezaji wa Taifa Stars kwenye kambini kwenye Hoteli ya TANSOMA, Dar es Salaam.
Nahodha huyo wa zamani wa Taifa Stars, alizitaka safu za ulinzi, kiungo na ushambuliaji kufanya kazi kwa umakini ili ushindi upatikane.
“Sioni sababu ya kupoteza mechi hii, lazima tushinde ili kuwapa matumaini Watanzania mara ya mwisho ukweli mlicheza vizuri sana na Ivory Coast na kila mtu alifahamu hivyo ingawa tulifungwa,” alisema Tenga.
Tenga amewataka wachezaji kutokurudia makosa yaliyotokea katika mechi mbili za kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco na Ivory Coast.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru