Monday 30 June 2014

JK ateta na ujumbe toka Vietnam


NA MWANDISHI WETU
RAIS Jakaya Kikwete, jana alikutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka kampuni ya simu ya Viettel kutoka Vietnam, ukiongozwa na Le Dang Dung ambaye ni Makamu wa Rais wa Kundi la Kampuni za Viettel Group.
Kwenye mkutano huo uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Dung alifuatana na Tao Duc Thang ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shughuli za Kimataifa za Kampuni hiyo – Viettel Global.
Dung amemwelezea Rais Kikwete kuhusu mipango ya Viettel kuwekeza katika shughuli ya mawasiliano ya simu hasa kwa maeneo ya vijijini.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru