Thursday 16 April 2015

Askofu awashauri viongozi Dar


NA REHEMA MAIGALA
MWENYEKITI  wa Ushirika wa Wachungaji wa Kipentekoste Tanzania (PPFT), Askofu Pius Ikongo, amewashauri viongozi wa Jiji la Dar es Salaam, kubadilisha ratiba ya ufanyaji wa usafi barabarani.
Alisema wafanya usafi wanatakiwa  kufanya kazi zao  jioni, kuanzia saa 12, ili kuepukana na msongamano mbalimbali  ambayo inakwamisha utendaji wao wa kazi .
Akizungumza na Uhuru jana, Dar es Salaam, Pius alisema bado suala la usafi haliridhishi katika Jiji la Dar es Salaam, kwa sababu ya msongamano na foleni za magari .
Alisema usafi ukifanywa jioni, jiji litaonekana kuwa safi kila siku, hata magari ya kubebea taka  yataweza kufanya kazi mara tatu kwa siku.
 “Ratiba ya usafi lazima ibadilishwe, jiji linatakiwa kufanyiwa usafi jioni, ili kujiepusha na msongamano ya magari na watu inayosababisha usafi usafi usifanyike vile inavyotakiwa”alisema Pius.
Pius aliongeza ratiba hiyo ikibadilishwa, Jiji la Dar es Salaam litaonekana safi wakati wote kama ilivyo miji ya nchi za jirani.
 Alisema wafanyakazi hao wanatakiwa wawe barabarani  wakiwa wamevalia sare zao rasmi kwa ajili ya kulinda mazingira, hasa kwa watu wanaochafua kwa makusudi.
Pius alitolea mfano kwa nchi za jirani kama Afrika Kusini na Kenya kuwa ni nchi ambazo zinazofanya usafi jioni, hali  inayofanya miji katika nchi hizo kuwa safi.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru