Saturday 18 April 2015

Zimamoto Mwanza walilia vitendea kazi


NA PRISCA MSHUMBUSI, MWANZA
JESHI la Zimamoto na Uokoaji jijini hapa linakabiliwa na uhaba wa vifaa vya uokoaji wakati wa mafuriko, suala linalosababisha kupata wakati mgumu kipindi mafuriko.
Akizungumza na gazeti hili, ofisini kwake, jana, Kamanda wa kikosi hicho mkoa humo, Andrew Mbate, alisema wanapata tabu wakati wa uokoaji pindi mafuriko yanapotokea.
Mbate alisema jeshi hilo halina vifaa vya kutumia katika uokozi wakati wa mafuriko suala linalosababisha walazimike kutumia vifaa bandia kuweza kuwasaidia wahanga wa mafuriko.
ìTuna vifaa bandia ambavyo tunatumia kuweza kuwanusuru wahanga wa mafuriko navyo haviaminiki katika shughuli hiyo, ila tunafanya hivyo ili kuweza kuwasaidi kwa wakati huo,î alisema Mbate.
Alisema wakati wa mvua na mafuriko hasa maeneo ya mabondeni, yanaweza kutokea maafa na kuwataka wakazi wa sehemu hizo kuhama kwa kuwa vitendea kazi vilivyopo ni vya bandia ambavyo haviaminiki katika shughuli hiyo.
ìKwa tahadhari nzuri ni bora wakazi wa mabondeni watoke, hasa kwa hapa Mwanza maeneo ambayo yana shida ni Mabatini. Ni bora wakatoka mapema kwani mvua bado zinaendelea kunyesha,î alisema.
Pia aliiomba serikali kujenga mifereji imara inayoweza kupitisha maji kwa urahisi kuepusha mafuriko yanayotokana na maji ya milimani.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru