Thursday 16 April 2015

Manispaa ya Ilala yatoa tuzo katika shule zake


NA EMMANUEL MOHAMED
HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam, imetoa tuzo kwa shule za msingi na sekondari zilizofanya vizuri kitaaluma na uboreshaji wa mazingira kwa mwaka 2014, zilizoko kwenye wilaya hiyo.
Katika hafla hiyo, Shule ya Sekonsdari ya Zanaki, iliongoza na kupewa tuzo.
Aidha, Shule ya Sekondari Minazi Mirefu, iliipata tuzo ya uboreshaji wa mazingira.
Tuzo hizo zilitolewa kwa shule za serikali na zisizo za serikali zilizofanya vizuri katika mitihani ya darasa la nne,  darasa la saba na kidato cha nne.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymound Mushi, alikabidhi tuzo hizo jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Saalam, wakati maadhimisho ya siku ya elimu na kilele cha mazingira.
Mushi alisema mpango huo ulioanzishwa ni sehemu ya mikakati ya serikali katika Matokeo Makubwa Sasa (BRN).
Alisema utoaji wa elimu bora una uhusiano na usafi wa mazingira na kwamba inasaidia kuongezeka kwa ufaulu wa shule za wilaya hiyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu wilaya hiyo, Angela Marembeka, alisema utoaji wa tuzo hizo ni moja ya motisha na itasaidia kuchochea ufanyaji kazi stahiki.

1 comments:

  1. Honereni sana kwa shule zilizopata tuzo. Honeza bidii.

    ReplyDelete