Tuesday 21 April 2015

Tani 10,000 za chakula kutolewa kwa wahitaji


NA RACHEL KYALA
SERIKALI itagawa tani 10,000 za chakula kuwasaidia watu ambao wanakabiliwa na njaa kutokana na uhaba wa chakula katika baadhi ya maeneo nchini.
Hatua hiyo imetokana na zaidi ya watu 400,000 kukabiliwa na njaa wakiwemo 42, 414 ambao hawana uwezo kabisa wa kununua chakula na wametengewa kupatiwa tani 1,000 bure.
Hata hivyo, tani zingine 9,000 zinatarajiwa kuuza kwa sh. 50 kwa kilo kwa watu 381,722, ambao kwa kiasi wana uwezo wa kumudu kununua chakula kwa bei hiyo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usalama wa Chakula, Onasimbo Mpika, alisema jana kuwa wilaya zitakazohusika na mpango huo ni Korogwe, Monduli na Longido, Nzega, Same, Mwanga, Pangani, Magu, Kishapu, Bunda, Kwimba, Rorya na Shinyanga.
“Pamoja na wilaya hizo, yapo maeneo mmbalimbali nchini yenye uhaba wa chakula ambayo tayari yameshafanyiwa tathmini na hali kuonyesha kuwa yanastahili kupata chakula cha bei nafuu,” alisema. 
Alitoa mfano wa wilaya hizo kuwa ni Chamwino, mkoani Dodoma, ambayo watu 13,031 wanahitaji tani 312.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru