Thursday 16 April 2015

Hakuna tishio la ugaidi Mwanza-Mulongo


PETER KATULANDA, MWANZA
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Magessa Mulongo, amesema mkoa huo uko salama na hakuna tishio lolote la ugaidi.
Alisema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa imejipanga kukabiliana na tishio lolote linaloweza kujitokeza.
Mulongo aliwataka wananchi wa mkoa huo kuendelea na shughuli zao kama kawaida na wasiwe na hofu yoyote.
Alisema hayo jana mjini hapa wakati akitoa taarifa ya hali ya usalama ya mkoa huo kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Amina Makilagi, kwenye kongamano la vijana wanawake wa vyuo na sekondari.
“Kuna baadhi ya watu wachache wanasambaza taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Mwanza iko kwenye mipango ya kuvamiwa na magaidi, taarifa hizo si sahihi na hazina ukweli wowote,” alisema.
Hata hivyo, Mulongo aliwataka viongozi wa chama tawala na serikali, wasioweza kasi ya utendajikazi wa CCM, kuachia ngazi.
 Katibu wa Chama mkoani hapa, Miraji Mtaturu, aliipongeza jumuiya hiyo kutokana na kazi nzuri inayofanya.
Aidha, Amina alisema lengo la kongamano hilo ni kuwajengea uwezo na uelewa wa masuala mbalimbali vijana.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru