Wednesday 22 April 2015

Kilifu ataka makada wanaokubalika CCM


NA SOLOMON MWANSELE, MBARALI
MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi, amekiomba Chama kufanya tathimini ya watu watakaogombea nafasi mbalimbali za uongozi.
Aidha, alisema viongozi ambao hawakubaliki wasigombee tena na badala yake wateuliwe wanaokubalika.
Kilufi alisema hayo jana kwenye kikao cha kamati ya siasa ya Chama ya wilaya ya Mbarali, kilichohudhuriwa na Katibu wa Chama mkoa wa Mbeya, Mwangi Kundya.
Kundya yupo katika ziara ya kuzitembelea wilaya zote za Mkoa wa Mbeya na katika ziara hiyo ameambatana na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa, Bashiru Madodi.
Ziara hiyo ina lengo la kukagua uhai wa Chama na maandalizi ya uchaguzi mkuu.
Kifuli alisema ni lazima Chama kijipange vya kutosha kwa ajili ya kuwapata wagombea kwenye ngazi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi huo. 
“Katibu hata mimi nikionekani sifai basi nielezwe mapema, wananchi wa jimbo hilo wana imani kubwa na CCM, hivyo awekwe mtu anayefaa,” alisema.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru