Saturday 18 April 2015

UWT mkoani Arusha yawakataa walimu


NA SHAABAN MDOE, ARUSHA
UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Arusha umetangaza kuwakataa walimu kusimamia uchaguzi wa madiwani, wabunge na Rais.
Aidha umewanyooshea kidole baadhi ya askari kwa kuwa na mapenzi yaliyopitiliza dhidi ya wanasiasa, hali inayosababisha washindwe kutenda haki katika maamuzi mbalimbali.
Msimamo huo ulitangazwa kwa nyakati tofauti na Mwenyekiti wa UWT mkoani humo, Flora Zelote, alipokuwa akizungumza katika kata mbalimbali za Wilaya ya Arusha kwenye ziara ya kukagua uhai wa jumuia hiyo na Chama kwa ujumla.
Alisema kutokana na hali hiyo, UWT Arusha ina mpango wa kufikisha mapendekezo kwa Tume ya Uchaguzi na makao makuu ya Chama kuona namna ya kuwapata wasimamizi wengine wa uchaguzi mbadala wa walimu.
Mwenyekiti huyo alisema Chama Cha Mapinduzi kimeonekana kama mpangaji katika nyumba yake kutokana na mabaya yanayofanywa dhidi yake na watumishi wa umma, huku kikiendelea kukaa kimya.
Aidha alitumia nafasi hiyo kuwatahadharisha viongozi wa CCM taifa kurejesha majina ya wagombea yatakayopendekezwa toka mikoani.
Alisema hali ilivyo sasa Chama kinapaswa kuheshimu zaidi matakwa ya wananchi ya nani wanamtaka badala ya kuendelea ya kuwapendekeza watu kwa utashi wa wachache.
ì Nitoe msimamo wa jumuia yangu Mkoa wa Arusha, tutapendekeza wagombea kwa matakwa ya wananchi watakaowachagua na tutawafikisha kwao ili wafanye maamuzi sahihi, wakifanya vinginevyo wakawaleta wa kwao tutawapa taarifa waje kuwafanyia kampeni,î alisema Zelote.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru