Wednesday 22 April 2015

Kadi za kliniki zazusha balaa


Na Ahmed Makongo, Bunda
WANAWAKE katika Jimbo la Mwibara wilayani Bunda mkoani Mara, wameilalamikia hatua ya hospitali, vituo vya afya na zahanati za serikali na binafsi kuwauzia kadi za kliniki kwa gharama ya sh. 2,000.
Walitoa malalamiko hayo jana mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Joshua Mirumbe, ambaye yuko ziarani kuhamasisha shughuli za maendeleo na kukagua ujenzi wa maabara katika sekondari za kata.
Walidai baadhi ya wauguzi wa hospiali, vituo vya afya na zahanati katika jimbo hilo, wanawauzia wajawazito kadi za kliniki na kwamba, vitendo hivyo vimekuwa vikifanyika kwa muda mrefu sasa.
“Hapa wake zetu wakienda kliniki wanauziwa kadi ambazo zinatakiwa zitolewe bure hivyo tunakuomba utuondoshe kero hiyo,” alisema Stephano Sasta.
Kwa upande wake, Mirumbe alisema ataunda tume ya kufuatilia kero hiyo, ambapo alisema kadi za kliniki ni mali ya serikali na zinatolewa bure.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru