Wednesday 26 March 2014

Tatizo la maji kuwa historia Chalinze




KAMPENI ZA UBUNGE CHALINZE

NA MWANDISHI WETU

TATIZO la maji katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Chalinze litakuwa historia baada ya kuanzisha mradi wa kuchimba visima.
Mgombea ubunge wa CCM katika uchaguzi mdogo jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, alitoa ahadi hiyo jana katika kijiji cha Diozile wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo.
Alisema kuchimba visima ndilo suluhisho la haraka la kutatua kero ya maji ili wananchi ili waondokane na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo
Ridhiwani alisema awamu ya tatu ya mradi wa maji wa Wami inaelekeza kufikisha maji hadi kwenye vitongoji lakini mradi huo unawezekana ukachelewa bali huduma hiyo ni muhimu.

“Nitachimba visima viwili Diozile ili mama zangu waondokane na adha ya kufuata maji maeneo ya mbali kwenye lambo linalofahamika kama lambo la Kikwete,” alisema.
Aliahidi kushirikiana na wananchi wa kijiji hicho kujenga zahanati ili kina mama wapate huduma kina mama wapate huduma bora za afya  ya uzazi.
Mapema, Diwani wa Kata ya Msoga, Mohammed Mzimba, alisema maji na zahanati ni changamoto kubwa kwenye kijiji hicho.
Alisema wanawake wanakonda kwa kuchota maji hivyo kumuomba Ridhiwani akiingia bungeni, ajenda yake ya kwanza iwe maji.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru